Mshambuliaji
wa Azam FC, Didier Kavumbagu akishangilia na wenzake baada ya kuifungia bao la
kwanza wakati wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya El Merreikh ya
Sudan jana Februari 15,2015 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Mabingwa wa
Tanzania Bara 2013/2014, Azam FC wameanza kwa kishindo Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya
kuichapa El Merreikh kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar
es Salaam.
Mshambuliaji
Didier Kavumbagu alifungia Azam FC bao la kuongoza dakika ya 9, kabla ya Nahodha
John Bocco aliyeingia akitokea benchi kupachika bao la pili kwa mabingwa hao wa
Tanzania Bara na kujiweka katika mazingira mazuri ya kusonga mbele kabla ya
mchezo wa marudiano.
Ushindi huo
wa Azam FC umekuja ikiwa ni siku moja baada ya wawakilishi wengine wa Tanzania
katika Kombe la Shirikisho, Yanga SC kuichapa BDF XI kwa mabao 2-0 kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Jumamosi Februari 14,2015.
|
No comments:
Post a Comment