COPPA ITALIANA 2014/2015:-Hiki ndicho Kipigo Juventus walichokitoa kwa Verona usiku wa Januari 15,2015 sasa hao Robo Fainali na Parma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, January 16, 2015

COPPA ITALIANA 2014/2015:-Hiki ndicho Kipigo Juventus walichokitoa kwa Verona usiku wa Januari 15,2015 sasa hao Robo Fainali na Parma.

Mabingwa wa Italia, Juventus, wakicheza bila ya Nyota wao Carlos Tevez, Andrea Pirlo na Gigi Buffon, waliopumzishwa wakati Arturo Vidal akiwa mgonjwa, waliifumua Verona Bao 6-1 kwenye Mechi ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Coppa Italiana usiku wa Jana Januari 15,2015. 

Hadi Mapumziko Juve walikuwa mbele Bao 3-0 kwa Bao mbili za Sebastian Giovinco na moja la Roberto Pereyra.

Kipindi cha Pili, Paul Pogba akapiga Bao la 4 na kuifanya Juve iongoze 4-0 lakini Nene akafunga Bao kwa Verona na Gemu kuwa 4-1.

Alvaro Morata akaipa Bao la 5 Juve kwenye Dakika ya 63 kwa Penati baada ya Rafael Marquez kumwangusha Sebastian Giovinco na la 6 kufungwa na Coman.

Juve sasa wametinga Robo Fainali na watacheza Nyumbani na Parma ambayo iliifunga Cagliari 2-1.

Mechi za Robo Fainali zitachezwa Februari 4,2015.

Jumanne Januari 20,2015

2300 AS Roma vs Empoli

Jumatano Januari 21,2015

2000 Fiorentina vs Atalanta

2300 Inter vs Sampdoria

Alhamisi Januari 22,2015

2300 Napoli vs Udinese

Robo Fainali

Jumatano Februari 4,2015

AC Milan vs Lazio

Inter/Sampdoria vs Napoli/Udinese

AS Roma/Empoli vs Fiorentina/Atalanta

Juventus vs Parma

Nusu Fainali

Machi 4 & Aprili 8,2015

AC Milan/Lazio vs Inter/Napoli/Sampdoria/Udinese

AS Roma/Fiorentina/Empoli/Atalanta vs Juventus/Parma

Fainali

Juni 7,2015- Rome

UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad