LIGI KUU YA VODACOM 2014/2015:-Mabingwa watetezi Azam FC na Yanga SC wagawana Pointi leo Desemba 28,2014 Taifa…Tazama Taswira ya mechi ilivyokuwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 28, 2014

LIGI KUU YA VODACOM 2014/2015:-Mabingwa watetezi Azam FC na Yanga SC wagawana Pointi leo Desemba 28,2014 Taifa…Tazama Taswira ya mechi ilivyokuwa.

Wachezaji wa Yanga wakishangilia ushindi na Washabiki wao baada ya Yanga SC kugawana pointi na Mabingwa watetezi wa Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara 2013/2014,Azam FC kufuatia kufungana bao 2-2 kwenye mechi ya Ligi kuu leo Desemba 28,2014 uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

 Mshambuliaji wa Yanga SC,Hamis Tambwe aliipatia timu yake bao la kusawazisha katika mtanange wa  ligi kuu tanzania bara, kwa kichwa baada ya kuiwahi krosi ya Salum Telela huku Simon Msuva akifunga kwa kichwa kwa pasi ndefu ya Niyonzima na kufanya mchezo umalizike kwa bao 2-2.


Wachezaji wa timu ya Azam FC wakishangilia goli yao la kwanza dhidi ya Yanga.Azam FC magoli yao yamefungwa kupitia Kavumbagu  baada ya mabeki wa Yanga SC kuchanganyana na kipa Dida na Bocco kwa bao la kichwa kwa krosi safi ya Himid Mao.


Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) itaingia raundi ya tisa Januari 3 mwakani kwa mechi tano,kwa  Coastal Union itacheza na JKT Ruvu katika Uwanja wa Mkwakwani, Ruvu Shooting itaikaribisha Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mabatini, Azam itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Azam Complex, Stand United itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri wakati Mbeya City na Yanga zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Sokoine.

Ligi hiyo ambayo itachezwa mfululizo (non-stop) hadi itakapomalizika Mei 9 mwakani, itakamilisha raundi ya tisa Januari 4 mwakani kwa mechi kati ya Mgambo Shooting na Simba kwenye Uwanja wa Mkwakwani, na Tanzania Prisons itakayokuwa mwenyeji wa Ndanda kwenye Uwanja wa Sokoine.

Nayo mechi kati ya Mtibwa Sugar na Stand United ambayo jana ilivunjwa na mvua dakika ya 6 imemaliziwa leo ambapo timu hizo zimetoka sare ya bao 1-1.

Wakati huo huo, mechi ya ligi iliyochezwa jana usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex imemalizika kwa wageni Ruvu Shooting kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Ruvu. Bao hilo lilifungwa kipindi cha kwanza kwa mkwaju wa penalti uliopigwa na Hamisi Kasanga.  
 

UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad