Uwanjani
Stamford Bridge, Wenyeji Chelsea wameichakaza NK Marbor kwa kuichapa Bao 6-0
katika Mechi ya G.
Chelsea
walifungua kitabu cha Magoli Dakika ya 13 baada ya pasi safi ya John
Terry kumfungulia njia Loic Remy aliefunga vizuri na kuipa Chelsea Bao la
kuongoza.
Juhudi hiyo
ya Remy ilimfanya aumie Nyonga na Dakika chache baadae kutoka nje na nafasi
yake kuchukuliwa na Didier Drogba.
Drogba
aliipa Chelsea Bao la Pili katika Dakika ya 22 kwa Penati iliyotolewa baada ya
Pasi ya Willian kumgonga mkononi Ales Mertelj.
John Terry
aliipa Chelsea Bao la 3 katika Dakika ya 30 kufuatia kaunta ataki safi
iliyoanzia kwa Drogba kuokoa Mpira langoni wakati wa Kona na Eden Hazard
kukokota Mpira hadi eneo la Maribor na kumpasia Cesc Fabregas aliempa Terry,
aliepanda toka Difensi, na kufunga.
|
Dakika ya
54, Chelsea walipata Bao la 4 la kujifunga wenyewe kufuatia krosi ya Eden
Hazard kumgonga kwenye kisigino Mitja Viler na kutinga.
NK Maribor
walipata Penati katika Dakika ya 64 iliyotolewa baada ya Nemanja Matic
kumchezea Rafu Agim Ibraimi ambae alipiga mwenyewe na kugonga Posti.
Chelsea
walifunga Bao la 5 kwa Penati waliyopata baada ya Marko Suler kumshika
Branislav Ivanovic na kumwangusha na Penati hiyo kufungwa kifundi na Eden
Hazard katika Dakika ya 77.
Dakika ya
90, Eden Hazard aliipa Chelsea Bao la 6 baada kupokea na kutuliza pasi ya juu
toka kwa Nathan Ake na kumpunguza Beki mmoja na kufunga.
|
MSIMAMO.
|
RATIBA/MATOKEO
UEFA CHAMPIONS LEAGUE 2014/2015.
Jumanne Oktoba 21,2014.
KUNDI E
CSKA Moscow 2- 2 Man City AS Roma 1 – 7 Bayern Munich KUNDI F APOEL Nicosia 0 – 1 Paris St-Germain Barcelona 3 – 1 Ajax KUNDI G Chelsea 6 – 0 NK Maribor FC Schalke 4 – 3 Sporting Lisbon KUNDI H BATE Borisovs 0 – 7 Shakhtar Donetsk FC Porto 2 – 1 Athletic Bilbao |
MSIMAMO.
|
RATIBA/MATOKEO
UEFA CHAMPIONS LEAGUE 2014/2015.
Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku kwa Saa za Bongo. Jumatano Oktoba 22,2014. KUNDI A Atlético Madrid v Malmö FF Olympiakos v Juventus KUNDI B Liverpool v Real Madrid Ludogorets Razgrad v FC Basel KUNDI C Bayer 04 Levserkusen v Zenit St Petersburg Monaco v Benfica KUNDI D Galatasaray v Borussia Dortmund RSC Anderlecht v Arsenal |
Karibu
kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana
/Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
No comments:
Post a Comment