SOMA RIPOTI YAUNESCO:-Ni kuhusu Tanzania kuhitaji Walimu Laki nne ifikapo mwaka 2030. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, October 21, 2014

SOMA RIPOTI YAUNESCO:-Ni kuhusu Tanzania kuhitaji Walimu Laki nne ifikapo mwaka 2030.

Hii ni moja ya nyumba za Walimu wa shule ya Msingi Mihuga iliyopo Wilayani Bagamoyo. mazingira ya namna hii yanasababisha walimu wengi kuikimbia fani yao ya ualimu. Picha na Ibrahim Yamola

 Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO) hivi karibuni limetoa ripoti inayoonyesha Tanzania itahitaji angalau walimu 406,600, ifikapo mwaka 2030.

Wakati mahitaji ya walimu katika nchi mbalimbali yakizidi kuwa makubwa, shirika hilo linasema uhaba wa walimu wenye mafunzo unazidi kutamalaki katika nchi mbalimbali, ikiwamo Tanzania.

Kwa sasa na inawezekana na baadaye, Afrika ndiyo inayoongoza kwa kuwa na uhaba mkubwa wa walimu, jambo linalohatarisha mustakabali wa sekta ya elimu barani humu.

Ukiondoa Tanzania, ripoti hiyo inaonyesha mahitaji makubwa ya walimu pia yanazikabili nchi kadhaa za Afrika, zikiwamo Uganda, Nigeria na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Kwa ngazi ya dunia ripoti hiyo inasema hadi mwaka huo, walimu zaidi ya milioni 27 watahitajika kuziba mapengo ya walimu wanaostaafu na nafasi mpya za ajira.

Hata hivyo, taarifa nzuri ya ripoti hiyo inaonyesha kama Tanzania itajipanga vizuri, inaweza kuziba pengo la walimu , hasa katika shule za msingi ifikapo mwaka 2026.

 Hilo linawezekana ikiwa nchi hiyo itakuwa inaajiri angalau asilimia 10 ya walimu kila mwaka.

Hata hivyo, Unesco inasema mikakati ya kuziba mianya hiyo ya walimu katika nchi nyingi imegubikwa na dosari kubwa kwa vyombo husika kuajiri walimu wasio na mafunzo bora ya ualimu.

Takwimu zinaonyesha kuwapo kwa tatizo sugu la walimu wasio na mafunzo katika nchi nyingi. Kama hatua hazitochukuliwa, itakuwa vigumu kwa watoto wote kwenda shule na kujifunza,” inasema taarifa ya Unesco iliyotolewa kwa umma.

Karibu kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana /Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad