Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa
mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga akiongea na
waandishi wa habari (hawapo pichani) October 21,2014,juu ya sakata la umri halali wa Mrembo
alietwaa taji hilo Mwaka huu, Sitti Abbas Mtemvu ,katika mkutano huo
Lundenga alitolea ufafanuzi swala la umri wa Mrembo huyo kulingana na vilelezo
alivyopewa na mrembo huyo wakati akijiunga na mashindano hayo.
Yafuatayo ni
mambo waliyoyasema Hasheem Lundenga na Miss Tanzania 2014 Sitti.
‘Walidai
kwamba Miss Tanzania ana mtoto baada ya kutoka picha moja akiwa na mtoto,
nasema katika utafiti wetu sisi Miss Tanzania hana mtoto na mwenye vithibitisho
halali kwamba ana mtoto atuletee, kama kuna uthibitisho wa cheti cha kuzaliwa
cha mtoto….. leta hicho cheti’ –
‘Hili la
sisi kuchukua rushwa kutoka kwa baba wa Sitti, Abbas Mtemvu…. jamani hii ni
stori ya kijingajinga, ni mambo ya kipumbavu sana kuandika haya mambo, hamjui
taratibu zetu tunavyowapata majaji na wanavyofanya kazi…Majaji huwa wanatafutwa
siku nne za mwisho na huwa hakuna mtu anajua atakua Jaji na huwa tupeleka
majina 15 BASATA na wao ndio wanaturudishia majina tisa ya Majaji waliopitishwa’
–
‘Magazeti
mbalimbali yameripoti kwamba Sitti alikua na Masters, ukweli ni kwamba katika
fomu tulizonazo sisi Sitti hajaandika hata sehemu moja kwamba amesoma mpaka
Masters, swala la Masters limetoka wapi? ni uongo huo’ - Lundenga alisema.
‘Kuhusu
swala la yeye kuzungumza kifaransa, mtu anajua lugha ya kimataifa mbona kwenye
mashindano ya dunia wanazungumza Kifaransa na lugha nyingine? lakini mbona hata
kwenye fainali alijibu kwa Kiingereza pia? Kifaransa zilikua ni mbwembwe
kuwashawishi Majaji, na kweli walishawishika na ndio maana akashinda’ – .
‘Jingine
ambalo ni kubwa zaidi ni swala la umri lililozungumzwa sana, katika mashindano
yetu washiriki wote hujaza fomu na kuandika tarehe ya kuzaliwa, fomu ya Sitti
hii hapa na inaonyesha amezaliwa May 31 1991 kwa hiyo alitimiza masharti ya
kushiriki kwa kuwa ana umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 24′.
‘Wote
walioshiriki Miss Tanzania 2014 akiwemo Sitti walituletea vyeti vyao Original
vya kuzaliwa tarehe 13 na kisha tukatoa nakala kupitia hivyo vyeti vyao
Original’ – Lundenga aliongeza.
‘Sisi kazi
yetu sio kupeleleza sana, tukipata information chache zinatutosha… kama mtu
anatatizo na hiki cheti cha Sitti cha kuzaliwa akafanye utafiti, ukipata ukweli
tuletee sisi lakini kazi ya uchunguzi sio ya kwetu’
|
No comments:
Post a Comment