Kuna taarifa
ambazo kama ukibahatika zikakufikia, zinaweza kukuacha kinywa wazi ama
kukushtua kwa namna fulani.
Stori ambayo
nimeipata hivi punde kutoka 254 Kenya inahusiana na mazishi ya aina yake ambapo
familia moja imefanya mazishi ya mzee wao aliyekuwa akifahamika kwa jina la
Adriano Aluchio anayetajwa kuwa mzee wa kuheshimika kwenye jamii hiyo akiwa
amekaa ndani ya jeneza lilichongwa kwa namna ya kipekee tofauti na
ilivyozoeleka.
Baadhi ya
watu waliohojiwa kuhusiana na tukio hilo wamesema ni utamaduni wa jamii ya
kabila la Lughia kufanya mazishi ya namna hiyo kwa mzee aliyeheshimika, kwa
imani kuwa amefariki lakini anaendelea kuwalinda watoto wake pamoja na jamii
yake.
Moja ya
wazee katika jamii hiyo amenukuliwa akisema, “Mazishi kama hayo ya kumkalisha
marehemu yalianza tangu zamani sana wakati wa mfalme Nabongo Mumia, na sisi
tulitokea katika jamii hiyo, tukimzika amelala hatoridhika… Ataonekana
akitembea huku juu….”
Baada ya
mazishi hayo ya kipekee, walichukuliwa ng’ombe dume wawili na kupiganishwa juu
ya kaburi kama njia ya kufukuza mapepo wachafu, huku wanakijiji wakipongeza
kitendo cha mzee huyo kupewa mazishi ya hadhi.
Jamii ya
Waidakho katika kabila la Walughia wanoishi katika kaonti ya kakamega
wanajulikana sana kwa mchezo wao unaowavutia watalii eneo hilo la kuwapiganisha
Fahali na kuku Jogoo.
|
No comments:
Post a Comment