Baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Kamanda Kova.
Jeshi la Polisi
Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia mtu mmoja anayefahamika kwa jina la
Gunner Meena (40) mkazi wa Kinyerezi, Segerea, Dar es Salaam, kwa tuhuma
za kujifanya mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa .
Tukio la
mwisho lililomfanya akamatwe ni pale alipomtishia mfanyabiashara mwenye asili
ya Kisomali aitwaye Abdi Dalmar, ili ampe Tshs 25,000,000/= ama sivyo
angechukua hatua chini ya Sheria ya Usalama wa Taifa.
Aidha jeshi
hilo katika kuendesha oparesheni zake za kutokomeza ujambazi wa kutumia silaha
limefanikiwa kukamata bastola nne na shot-gun moja wiki hii.
Na Gabriel Ng’osha/GPL
|
No comments:
Post a Comment