UJUMBE WETU WA LEO:- Sawa mnajua kuongea, kutenda Je? - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, August 24, 2014

UJUMBE WETU WA LEO:- Sawa mnajua kuongea, kutenda Je?

Watanzania ni mabingwa wa kukosoa, mabingwa wa kujua vitu vizuri kwa wakati, lakini tatizo zaidi ni kwamba, hawa wanaoongea, siku moja waite waweke kwenye viti na wape nafasi ya kufanya hili wanaowalalamikia.

Hapo kinaweza kutoka kitu cha ajabu mpaka ukabaki unajiuliza, waliokuwa wakilalamika ndiyo hawa kweli niliowapa nafasi, au walikuwa wanatumwa na mtu anayejua na wao walikuwa wasemaji tu? 

Somo langu kubwa na zuri ninalotaka mlielewe ndugu zangu kwa leo ni kwamba, si kila anayeongea sana anajua kutenda. 

Kutenda na kuongea ni vipaji viwili tofauti, ambavyo viko vichwani mwa watu wawili tofauti.

Tafakari zaidi, kisha ukimaliza, hatua zinakusubiri.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad