BIDII/MAFANIKIO:-Hiki ndicho kiwango cha Pesa anachopata Msanii Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kwa sasa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, August 24, 2014

BIDII/MAFANIKIO:-Hiki ndicho kiwango cha Pesa anachopata Msanii Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kwa sasa.

Tangu mwaka 2011, tulifahamu kuwa Diamond Platinumz ndiye msanii wa Tanzania anaelipwa kiasi kikubwa cha pesa, na mwaka jana 2013, ikaelezwa kuwa bila Milioni 10 au Milioni 8 za Kitanzania humpati kwenye show yako.

Lakini kiwango kipya kilichotajwa Agosti 22,2014, kitawapa kizunguzungu zaidi hasa mapromota wenye mitaji midogo wenye ndoto za kufanya kazi na mwimbaji huyo.

Kwa mujibu wa Meneja wake Babu Tale, hivi sasa kiwango cha chini anachochaji kwa show moja hapa nchini ni Dola elfu 15 (sawa na shilingi Milioni 25 za Tanzania).

Tuna show Marekani show kumi na tano (15), show kumi na tano dola elfu ngapi? Na kwa hapa Tanzania hatufanyi show chini ya dola e15,000.”  Babu Tale aliiambia Bongo5.

Kwa mujibu wa Babu Tale, wanachaji kiasi cha hadi dola 25,000 kwa show moja za nje ya nchi (ikiwemo Marekani).

Tunalipwa milioni 20 show moja, tunalipwa dola elfu 25,000 show moja, hii ni zaidi ya madawa ya kulevya.” Alisema wakati akikanusha tuhuma kuwa Diamond anauza dawa za kulevya.

Kwa mahesabu ya haraka haraka, shows 15 mara dola 25,000 ni sawa na  Dola Laki 375,000 (Sawa na shilingi za Tanzania Milioni 625,687,500).

Kama ni kweli, basi Diamond anastahili kweli kuitwa Dangote wa Bongo Flava.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad