UEFA CHAMPIONZ LIGI 2014/2015:- Timu 5 zimesonga hatua ya Makundi ya UEFA ,Leo Agosti 27,2014 ….Ni shidaaaaaa kwa Arsenal kufuzu?? - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, August 27, 2014

UEFA CHAMPIONZ LIGI 2014/2015:- Timu 5 zimesonga hatua ya Makundi ya UEFA ,Leo Agosti 27,2014 ….Ni shidaaaaaa kwa Arsenal kufuzu??

Leo Agosti 27,2014,Usiku, Arsenal wanatinga Uwanjani kwao Emirates kurudiana na Klabu ya Uturuki Besiktas kwenye Mechi ya Raundi ya Mwisho ya Mchujo ya UEFA CHAMPIONZ LIGI 2014/2015.

 Wiki iliyopita huko Instanbul, Besiktas na Arsenal zilitoka 0-0 na Arsenal wanahitaji ushindi tu ili kufuzu kwani Sare yeyote ya Magoli itamaanisha Besiktas ndio wataingia hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ambayo Droo yake itafanyika huko Monaco Siku ya Alhamisi Agosti 28,2014.

Arsenal wanaingia kwenye Mechi hii bila ya Kiungo wao mahiri Aaron Ramsey ambae alipewa Kadi Nyekundu kwenye Mechi ya Kwanza huko Instanbul.

Pia Arsenal itamkosa Nahodha wao Mikel Arteta mwenye tatizo la Enka na vile vile kumkosa Straika wao Olivier Giroud ambae pia ameumia Enka.

Kukosekana kwa Giroud kunaweza kutoa namba kwa Chipukizi Yaya Sanogo au Lukas Podolski au hata Alexis Sanchez kuchezeshwa kama Sentafowadi au ikibidi, Arsene Wenger kumtumia Joel Campbell.

Wakati Besiktas wana Kikosi kamili na Straika wao Demba Ba yu tayari kurejea tena Jijini London kuitesa Arsenal kama alivyokuwa akifanya akiwa na Klabu yake ya zamani Chelsea, Klabu hiyo ya Uturuki itakuwa bila ya Meneja wao kutoka Croatia kwenye Benchi, Slaven Bilić, ambae alipewa Kadi Nyekundu katika Mechi ya Kwanza na hivyo kulazimika kukaa Jukwaani kwa Mechi hii.

**Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku**Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza.

Jumatano Agosti 27,2014.

Arsenal v Besiktas [0-0]

Athletic Bilbao v Napoli [1-1]

Bayer 04 Leverkusen v FC Copenhagen [3-2]

Ludogorets Razgrad v Steaua Bucharest [0-1]

Malmö FF v FC Red Bull Salzburg [1-2]

Aidha Usiku wa jana Agosti 26,2014,Timu 5 zimesonga hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI 2014/2015, baada ya kushinda Mechi zao za Marudiano lakini Celtic, ambao walifika hapa kibahati, wametupwa nje baada ya kuchapwa kwao Bao 1-0 na NK Maribor ya Slovenia.

**Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili.

Jumanne Agosti 26,2014.

Zenit St Petersburg 3 Standard Liège 0 [4-0] 

Apoel Nicosia 4 Aalborg BK 0 [5-1]

BATE Borisov 3 Slovan Bratislava 0 [4-1]

Celtic 0 NK Maribor 1 [1-2]

FC Porto 2 Lille 0 [3-0]

Timu 10 ambazo zitashindwa kwenda Makundi ya UEFA zitatupwa kwenye Mashindano ya UEFA EUROPA LIGI 2014/2015 hatua ya Makundi.

KLABU ZITAKAZOANZA HATUA YA MAKUNDI.

[Klabu 22]

-Atlético Madrid
-Barcelona
-Real Madrid
-Bayern Munich
-Borussia Dortmund
-Schalke 04
-Sporting CP
-Paris Saint-Germain
-Monaco
-Olympiacos
-Manchester City
-Juventus
-Shakhtar Donetsk
-Liverpool
-AS Roma
-Chelsea
-Benfica
-Ajax
-CSKA Moscow
-Galatasaray
-Anderlecht
-FC Basel

**ZITAUNGANA NA TIMU 10 ZITAKAZOFUZU KUTOKA RAUNDI YA MWISHO YA MTOANO NA KUINGIZWA DROO YA KUPANGA MAKUNDI 8 YA TIMU 4 KILA MOJA
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad