BUSARA:- Soma hiki ‘’Khadija Omary Kopa’’alichowachana Wasioheshimu Waume. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, August 27, 2014

BUSARA:- Soma hiki ‘’Khadija Omary Kopa’’alichowachana Wasioheshimu Waume.

MALKIA wa muziki wa Taarab Afrika Mashariki, Khadija Omary Kopa amewachana mastaa wa kike wasioheshimu waume zao kwa usupastaa wao, akisema suala hilo limewafanya washindwe kudumu katika ndoa zao.

 Malkia huyo alitoa dongo hilo juzikati wakati alipokuwa akipagawisha mashabiki wake katika ukumbi wa Meeda uliopo Sinza Mori jijini Dar alipokuwa jukwaa moja na bendi ya Extra Bongo, akiimba nyimbo zake mbili za Fahari ya Mwanamke na Full Stop.

Mwanamke unajiona staa mbele ya mumeo kisa supastaa, eti inafikia hatua  hadi unaachika! mwanamke unapaswa uwe na heshima kwa mumeoeeee!”alisema mkali huyo na kuitikiwa kwa shangwe na mashabiki wake kibao waliokuwa wakimshangilia kwa nguvu.

Stori:- Shakoor Jongo
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
 Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad