MAENDELEO/CHANGAMOTO:-Taswira ya Yaliyojiri katika Kongamano la Dini ya Kiislamu kwa nchini za Africa Mashariki na Kati Nchini Burundi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, August 20, 2014

MAENDELEO/CHANGAMOTO:-Taswira ya Yaliyojiri katika Kongamano la Dini ya Kiislamu kwa nchini za Africa Mashariki na Kati Nchini Burundi.

Baadhi ya viongozi wa kiislamu kutoka nchi za Afrika Mashariki na kati wameshauriana kuelimisha jamii katika nchi hizo  kuepukana na dhana mbaya inayoenezwa na baadhi ya watu kuwa dini ya kiislamu ni dini ya Kigaidi.

 Akifungua Kongamano la kidini la Agosti 15 hadi 17,2014, katika Jiji la Bujumbura nchini Burundi,Mufti wa nchi hiyo Shekhe Sadick Kajande alisema dhana inayoenezwa ya waislamu kuwa magaidi inasababisha watu kutoaminiana katika shughuli za maendeleo. 

Shekhe Kajande alisema kuwa dini ya kiislamu inahamasisha umoja amani na mshikamano na kukataza mabaya kulingana na sheria za Mungu na hata za kiserikali ambazo hazikubaliwi ikiwa ni pamoja na kutojihusisha na mauaji.

Alisema kuwa kinachotakiwa kwa waumini wa kiislamu ni kujihadhari na hamaki kutoka kwa baadhi ya watu wanahamasishana kuuchafua uislamu bali wazingatie misingi ya imani zao pamoja na kuzingatia sheria za nchi wanakoishi.

 Aidha shekhe Mrisho Kasimu kutoka kivu ya kaskazini (DRC) amesema kinachotakiwa kufuatwa ni misingi ya imani za dini hiyo kwa kuamini mungu mmoja malaika wake vitabu na mitume iliyowekwa na Mwenyezi Mungu.

Alisema kuwa imani nyingine ni kuamini kuwepo siku ya kifo kwa matashi ya allha na kwamba kila jema na baya ni kutokana na kudra zake muumba ambapo katika kuzingatia Q’urani lazima nguzo tano za kiislamu zisimamiwe ipasavyo.

Akichangia  hoja ya Maendeleo ,Shekhe Mohamad Gamaga kutoka nchini Uganda alisema waislamu wasisitize vizazi vyao na jamii zinazowazunguka  kuondoa changamoto za elimu ,afya na amani kwa kupinga uhalifu unaohatarisha usalama.

Gamaga aliwaomba waislamu wa mataifa mbalimbali kufuata sunna za mtume na sheria za nchi zao ili mradi zile ambazo haziwazuii kufanya ibada zao kwa Mujibu wa sheria na wao  wasitumie dhana inayoenezwa kujihusisha na uvunjifu wa Amani.

Katika kongamano hilo waumini na viongozi kutoka nchi  za Tanzania, Uganda , Rwanda Burundi na DRC wamechanga kiasi cha  Faranga Milioni tatu kwa ajili ya kujenga Hospitali ya wanawake  nchini Burundi ili  kupata sehemu ya kujifungulia watoto wao.

Pamoja na mambo mengine,Waumini hao  wamekubaliana kukutana mara kwa mara kujadili changamoto za kiimani   na kuweka mikakati ya kujenga Shule na Hospitali za kidini  kwa nchi wanachama ambapo kongamano lingine litafanyika Desemba Mwaka huu nchini Uganda.
Ni Viongozi wa kiislamu kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati walipokutana katika Jiji la Bujumbura nchini Burundi  Agosti 15 hadi 17,2014,katika uwanja wa Nyakabiga wakati wa kongamano la siku 3 lenye lengo la  kujadili mikakati ya Maendeleo na Changamoto za  Uislamu Duniani.
Kutoka kushoto ni Mpatanishi wa Amani katika Serikali ya Burundi ,Shekhe Mohamed Abdul Rukala ,wa pili ni Mufti wa Burundi,Shekhe Sadick kajande na Shekhe Funga Njia Salim kutoka Kivu ya Kaskazini-DRC.
Mwana Matukio wetu Ustadhi Shaaban Nasib Ndyamukama nae alihudhuria kongamano hilo la Agosti 15 hadi17,2014.
Shekhe Funga Njia Salim kutoka Kivu ya Kaskazini ,akichangia moja ya mada kuhusu Changamoto za Uislam na Maendeleo.
....Shekhe Mohamad Gamaga kutoka nchini Uganda...
 Baadhi ya Waumini wa kike wa dini ya Kiislam wakiwa wamekaa kwa utulivu wakati walipokutana wakitokea katika nchi za Rwanda, Burundi ,Uganda ,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Tanzania (Mkoani Kagera) wakati wa kongamano la siku 3-Agosti 15 hadi 17,2014 kuhusu  kujadili mikakati ya Maendeleo na Changamoto za Kidini kwenye uwanja wa Nyakabiga nchini Burundi.Picha/Habari Na:-Shaaban Ndyamukama.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0789-925-630.
 
Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad