Kama nia ni
kufanya niishi maisha ya uoga, kudhoofika na msongo wa mawazo mmefeli ,,,,,
wengine mkijidai ni wacha Mungu huku mkiumiza nafsi za watoto wa binadamu
wenzenu.
No wonder mnaishi bila amani mbali na utajiri mlionao kwa kuogopa visasi.
Sikuzaliwa
kukata tamaa
Pia wapo wanaopenda kuandikwa kwenye hayo magazeti yenu
Wafanyieni favor ya kuwapa hiyo nafasi mi sifanyi muziki wa magazeti ya udaku
Mkiachana na mimi nitashukuru sana
Hata ndoa
yangu ikivunjika haimaanishi mnitafutie story za kunichafua
Ndoa ya Madiba ilivunjika sembuse yangu nina utofauti ipi na binadamu wengine?
Nyie ndoa zenu ziko perfect si ndio?
Hewala watakatifu nyie, mnaoficha yenu na kutangaza ya wenzenu.
Mwisho
nawaomba watu mnaonielewa kutoamini tu habari yoyote ambayo haijatoka kwangu
wala kwa muwakilishi wangu ambae ni "Webiro Wakazi Wasira".
Kama kuna chochote cha watu kujua nitakiongea mimi kwa mdomo wangu sio kuwekewa
maneno mdomoni.
Kila siku
ooooh tulimpigia simu hapatikani, namba yangu yenyewe kwanza hata mnaijua???
Mngekuwa mnaijua msingekuwa mnahangaika mnawapigia watu wangu wa karibu
kunitafuta , na hao watu hawawezi kunisaliti ndio sababu mpaka miaka 70
mtaishia kusema tulimpigia simu JayDee hapatikani.
Nyie muongee chochote mnachojiskia
Ila sie hatuna haki kujitetea ??
Hili nalo
litapita kama mengine
Na inshallah nitakuwa hapa hapa nimesimama nawaangalia
|
No comments:
Post a Comment