Kipa Salim Magoola akiwa amebebwa
baada ya kupangua penalti ya Leonel Saint-Preux.
Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam
FC, Leo hii Agosti 20,2014,wametupwa nje ya Mashindano ya Klabu Bingwa ya
Afrika Mashariki na Kati, Kagame Cup2014, huko Kigali, Rwanda baada kutolewa
kwa Mikwaju ya Penati 4-3 na El Merreikh ya Sudan kufuatia Sare ya 0-0.
Mechi hi ilikuwa ni ya Robo Fainali
na sasa El Merreikh imesonga Nusu Fainali ambapo watacheza na Mshindi kati ya
KCC ya Uganda na Atlabara ya South Sudan zinazokutana baadae hii Leo.
Nusu Fainali nyingine itakuwa kati
ya Klabu za Rwanda, Polisi na APR, ambazo nazo zilishinda Mechi zao za Robo
Fainali kwa Mikwaju ya Penati hapo Jana Agosti 19,2014.
|
No comments:
Post a Comment