SOMA UTAFITI:-Kaswende, Mawazo, vyaweza kukusababishia uwe na Kipara.'' - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, July 25, 2014

SOMA UTAFITI:-Kaswende, Mawazo, vyaweza kukusababishia uwe na Kipara.''


Siyo wote wenye vipara mitaani vinatokana na uasilia. wengine ni kutokana na magonjwa na wengine ni mawazo…..Wataalamu mbalimbali duniani wamefanya utafiti juu ya sababu, chanzo na tiba ya tatizo la upara na haya ndiyo mambo waliyobaini. Picha Na:- Maktaba.

Kipara ni kitu ambacho kinawapata watu wengi walioko sehemu mbalimbali duniani. 

Takwimu zinaonyesha kuwa takriban asilimia 50 ya wanaume kwa nyakati tofauti maishani mwao hujikuta wanapata kipara.

Kwa wanaume, mara chache kipara, kinaweza kuanza mapema kati ya umri wa miaka 14 na 20, lakini wanaume walio wengi hupata kati ya umri wa miaka 30 na 60.

Wanaume wanaopata kipara huanza kuona nywele zikipungua kichwani hatua kwa hatua, kuanzia upande wa mbele au katikati ya kichwa na hatimaye sehemu hiyo huwa haina nywele kabisa.

Ingawa kimsingi kipara hufikiriwa kuwa ni tatizo la kawaida kwa wanaume, wanawake pia wanaweza kukabiliwa na tatizo hili. 

Inasemekana kuwa karibu asilimia 40 ya wanawake nchini Marekani, kutokana na sababu mbalimbali wana tatizo la kipara au kunyonyoka nywele kichwani.

Kila unywele huota na kukua katika kifuko cha nywele kiitwacho kinyweleo kilichoko kwenye ngozi.

Chini ya kila kinyweleo kuna kituta ambacho hushikilia unywele na kituta hiki hujulikana kama foliko ya nywele.

Katika hali ya kawaida wastani wa nywele 50 hadi 100 huchomoka kila siku kutoka katika vifuko vyake katika ngozi ya kichwani na kuanguka chini.

Jambo hili linaweza kugunduliwa kwa urahisi kwa kuona nywele kwenye vitana, chanuo au foronya tunazotumia wakati wa kulala.

Nywele zinapochomoka kwa wingi kuliko kawaida kila siku au zisipoota na kukua ili kuziba pengo la nywele zilizotoka, baada ya muda mtu huwa na kipara. Wakati mwingine nywele hupungua bila kutoka kichwani.

Hali hii inaweza kusababishwa na kupungua kwa unene wa unywele au kutofautiana kwa kasi ya kukua kwa nywele.

Ingawa chanzo hasa cha upara hakifahamiki vizuri, wanasayansi wanasema kuwa kukosekana kwa usawaziko sawia wa homoni ya kiume ya androjeni aina ya dihydrotestosterone (DHT) mwilini, ni moja ya vyanzo vya tatizo hili.

Homoni hii inapoongezeka mwilini hasa katika ngozi ya kichwa, husababisha mgandamizo wa ngozi ya katikati ya kichwa na kuathiri foliko za nywele kwa kuzifanya ndogo kiasi kwamba zinapoteza taratibu uwezo wake wa kutokeza nywele mpya.

>>ZAIDI SOMA HAPA:->>>http://www.mwananchi.co.tz/Kaswende-na-mawazo-/-/1596774/2397232/-/item/1/-/6icdcc/-/index.html

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad