AJALI:-Tazama Ajali ya Fuso iliyoua Watu watatu na Majeruhi Zaidi 47. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, July 25, 2014

AJALI:-Tazama Ajali ya Fuso iliyoua Watu watatu na Majeruhi Zaidi 47.


Lori lenye namba za usajili T680 ARL aina ya Fuso lililokuwa limepakiza mizigo na wafanyabiashara ambao idadi yao bado haijajulikana  likitokea kijiji cha Kiloleli wilayani Kishapu kwenda katika mnada wa Mhunze uliopo Kishapu,Mkoani Shinyang'a likiwa katika eneo la tukio katika kijiji cha Usunga kilometa chache kufika eneo la mnada.


Wakazi wa kijiji cha Uchunga wakiwa katika eneo la tukio leo…Wafanyabiashara watatu wamepoteza maisha na wengine 46 wamejeruhiwa vibaya.

Watu 3 wamekufa na wengine zaidi ya 47 wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kwenda mnadani kupinduka wilayani Kishapu Mkoani Shinyang'a.

Ajari hiyo imetokea  asubuhi katika eneo la uchunga wilayani humo baada ya gari hilo haina ya fuso namba T 680 ARL kuacha njia na kupinduka.

Chanzo cha ajari hiyo ni mwendo kasi na derava wa gari hilo aliyetambulika kwa jina la Shija Ngassa amekimbia  baada ya ajari hiyo.

Ajari hiyo ya fuso imesababisha vifo vya watu watatu ambapo moja ametambulika kwa jina la Difa Shimo  mili ya marehemu imehifadhiwa kwenye hospitali ya mkoa wa Shinyang'a.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Shinyang'a kamishina msaidizi wa polisi Jastus Kamugisha amethibitisha kutokea kwa ajari hiyo.

Kamugisha amesema jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo pamoja na kumsaka dereva wa gari hilo sanajali na kutoa onyo kwa wafanya biashara wa minadani kuacha kupanda magari ya mizigo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad