![]() |
Shilole ambaye
ni mmoja wa ‘Wasanii waliopewa Onyo na Serikali kuhusu kufanya sanaa ambazo
hazifati maadili’.
|
![]() |
.....Ney wa Mitego...... |
![]() |
........Wema Wema na Aunt
Ezekiel......
|
![]() |
Naibu waziri
wa Habari Utamaduni na Michezo ,Bw.Juma Nkamia akiwa na Waziri mkuu Mizengo
Pinda Bungeni mjini Dodoma.
|
Naibu waziri
wa Habari Utamaduni na Michezo ,Bw.Juma Nkamia akijibu swali la Catherine
Magige kuhusiana na udhalilishaji wa Wanawake unaofanywa kwenye kumbi mbalimbali
za starehe Tanzania…Waziri Nkamia alisema ‘nakubalia kabisa kwamba kumbi za
starehe zimekua zikitoa burudani na ajira kwa vijana hapa nchini lakini ndani
ya kumbi hizo kumekua na vitendo vinavyofanyika kinyume na maadili ikiwemo
udhalilishaji wa Wanawake’
‘Katika
kukomesha hali hiyo serikali kupitia baraza la sanaa BASATA wamefanya vikao
kadhaa na wamiliki wa bendi, maafisa utamaduni, wakuu wa polisi, wamiliki wa
kumbi na wanaojihusisha na uchezeshaji wa mtindo wa kanga moja ili kujadili
ukiukwaji wa maadili kwenye sanaa’.
Waziri
anasema ‘Pia serikali imeacha kutoa usajili kwa vikundi kama cha kanga moko kwa
kuwa uchezaji wake unakwenda kinyume na maadili ya Tanzania na kutoa onyo kwa
wamiliki wa kumbi, Wasanii na hata asasi zinazojihusisha na sanaa ambazo
hazifati maadili’.
Anasema
‘Wasanii waliopewa Onyo ni Ney wa Mitego, Shilole, Wema Sepetu, Aunt Ezekiel na
kwa upande wa kumbi ni Mama’s and Papa’s lakini pia maonyesho ya urembo ya Miss
Utalii yalifungiwa ambapo pia Serikali imeunda kamati ya kitaifa ya kuzuia
ukatili na unyanyasaji dhidi ya Wanawake/Wasichana watoto’
No comments:
Post a Comment