KUWA MSAFI:-Zaidi ya wanaume elfu 4 wamefanyiwa tohara katika Hospitali ya Nyamiaga wilayani Ngara mkoa wa Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, June 05, 2014

KUWA MSAFI:-Zaidi ya wanaume elfu 4 wamefanyiwa tohara katika Hospitali ya Nyamiaga wilayani Ngara mkoa wa Kagera.


Zaidi ya wanaume elfu 4 na mia 6 wamefanyiwa tohara katika Hospitali ya Nyamiaga wilayani Ngara wakati wa zoezi linaloendeshwa na wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia ofisi ya Mganga mkuu wa mkoa wa Kagera.


Zaidi ya wanaume elfu 4 na mia 6 wamefanyiwa tohara katika Hospitali ya Nyamiaga wilayani Ngara wakati wa zoezi linaloendeshwa na wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia ofisi ya Mganga mkuu wa mkoa wa Kagera.

Mratibu wa zoezi hilo Bi  Merisa  Lutayabulwa  amesema hayo  wakati akizungumza na Radio Kwizera kuhusu Mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa zoezi la la tohara kwa Wanaume lililoanza May 19,2014 hadi June 05,Mwaka huu kabla ya kuhamia  katika Zahanati ya Mukatabo  katika kata ya Kirushya wilayani Ngara.

Bi Lutayabulwa amesema licha ya wanaume wengi kujitokeza kupata huduma hiyo lakini changamoto kadhaa zimejitokeza ikiwemo baadhi ya watu kurudi tena hospitali wakiwa wanavuja damu kutokana kushindwa kufuata maelekezo waliyopewa awali baada ya kufanyiwa tohara.
 
Mmoja wa Wazazi waliowapeleka watoto wao kufanyiwa tohara Hospitalini hapo Bw Timotheo Christopher ameipongeza serikali kwa kufikisha huduma hiyo wilayani Ngara,mkoani Kagera.

Habari Na:-Radio Kwizera FM-Ngara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad