KUNYWA SUMU:-Aliyetaka kujiua kwa Wivu wa Kimapenzi wilayani Ngara mkoani Kagera,akana Shitaka Mahakamani…’’ - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, June 03, 2014

KUNYWA SUMU:-Aliyetaka kujiua kwa Wivu wa Kimapenzi wilayani Ngara mkoani Kagera,akana Shitaka Mahakamani…’’

……….Moja ya aina za sumu ya panya....Picha Na:-Maktaba Yetu......
Msichana  mwenye umri wa miaka 18 mkazi  wa  Musoma mkoani Mara  amefikishwa  katika mahakama ya wilaya ya Ngara akishitakiwa kwa kutaka kujiua kwa kunywa sumu ya panya  kwa kile kilichodaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.

Mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo,Andrew Kabuka, mwendesha mashitaka wa Polisi Bw George Gorotho amemtaja Msichana huyo kuwa ni Rosemary Masaru mkazi wa Musoma mjini mkoani Mara.

Bw Gorotho ameiambia Mahakama kuwa mshitakiwa huyo anadaiwa kutaka kujiua katika tukio la May 28,mwaka huu,majira ya saa 7 mchana katika shule ya Sekondari ya Ntobeye ,jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Mtuhumiwa amekana shitaka linalomkabili na yuko nje kwa dhamana  ya  Sh laki 5 baada ya kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni kuwa na mdhamini ambaye ni mtumishi wa serikali na mkazi wa wilaya ya Ngara ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi June 17 mwaka huu.

Katika hatua Nyingine, Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 anayesoma katika shule ya Sekondari Kanazi wilayani Ngara,mkoani Kagera amehukumiwa na Mahakama ya wilaya hiyo kutumikia adhabu ya kuchapwa viboko 9 baada ya kumkuta na na makosa mawili ambayo ni ubakaji na kusababisha ujauzito

Mbele ya hakimu wa wilaya ya Ngara Bi Mariam Rusewa, Mwendesha mashitaka wa Polisi ,Bw Tumaini Membi amemtaja mshitakiwa kuwa ni Jady Miburo mwenye umri wa miaka 17 ambaye ni mkazi wa Mukirehe wilayani Ngara
 

Habari na :-Radio Kwizera FM.-Ngara
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad