SOMA:-Utafiti: Ngono ya mdomo ni hatari na asilimia 20 ya saratani ya koo husababishwa na‘Oral Sex”. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, February 05, 2014

SOMA:-Utafiti: Ngono ya mdomo ni hatari na asilimia 20 ya saratani ya koo husababishwa na‘Oral Sex”.

Namna mdomo unavyoharibika kutokana na ngono kufanywa kwa kutumia mdomo. Picha ya Maktaba. ..Baadhi ya watu ambao wanakumbwa na ugonjwa huu shingo huvimba kama hivi. …Hata hivyo wapo wenye kuvimba hivi lakini si kwa sababu walifanya ngono kwa kutumia mdomo, isipokuwa yaweza kuwa ni sababu nyingine zikiwemo kurithi. ..Wataalamu wa masuala ya afya wanashauri kwamba ni muhimu sana watu wakaachana kabisa na tabia hii kutokana na ukweli kwamba siyo tu kwamba ni hatari kwa afya, pia ni sawa na kujiua mwenyewe, kwani kitendo hicho kinachangia magonjwa mengi.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini umeonyesha asilimia 20 ya saratani ya koo husababishwa na ngono ya mdomo maarufu kama ‘Oral Sex”.

Utafiti huo unaonyesha saratani ya koo licha ya kuambukizwa na njia mbalimbali ikiwemo ulaji wa vyakula vyenye pilipili, pombe kali, vitu vyenye uchachu pamoja na kurithi kutoka kwa wazazi.

Utafiti unaonyesha watu wengi hasa vijana wanamejiingiza kwenye vitendo hivi vya kufanya ngono wakitumia midomo hasa  ndimi, hivyo kuhatarisha uhai wao.

Katika utafiti  huo wa hivi karibuni, ulibaini wanaume 747  na wanawake wakiwa 472 hugundulika kila mwaka kuwa na saratani hiyo huku wanaopoteza maisha kila mwaka ni wanaume 444 wakifuatiwa na wanawake 270 kutokana na ugonjwa huo.

Utafiti unabainisha kuwa asilimia kubwa ya vijana wenye umri kati ya miaka 20 hadi 45 wanatumia staili ya kuwanyonya wenza wao sehemu za siri lengo likiwa ni  kuwavutia wapenzi wao katika  kushiriki ngono.

Vijana  wenye umri huo ndio wahanga wakubwa kwa sasa kutokana na ugonjwa huo kuonekana kuwaathiri kwa kasi, huku wengi wakiwa hawajui athari zake. 

Baadhi hujisifia kwamba ni wajuzi, kumbe wanajitafutia kifo kwa kufanya vitendo hivyo.

Utafiti unaonyesha kwa watu wazima walio wengi hawana muda wa kufanya hayo wanayofanya vijana, hivyo kujikuta angalau wanakuwa salama na kupatwa na saratani ya koo kwa njia hiyo inayoonekana kama ni chafu pia.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad