Wakati Kesi ya Zitto Kabwe kudai kurejeshewa nyazifa zake Februari 13, mwaka huu,Wakili wa chama cha CHADEMA,Tundu Lisu ameeleza kutoridhika na maamuziki ya Mahakama,hivyo Zitto Kabwe atabaki kuwa Mbunge wa Mahakama. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, January 08, 2014

Wakati Kesi ya Zitto Kabwe kudai kurejeshewa nyazifa zake Februari 13, mwaka huu,Wakili wa chama cha CHADEMA,Tundu Lisu ameeleza kutoridhika na maamuziki ya Mahakama,hivyo Zitto Kabwe atabaki kuwa Mbunge wa Mahakama.


Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe akiwa ndani ya Mahakama Kuu akisubiri hukumu ya kesi yake leo(Januari 07,2014).


Mwanasheria wa Zitto Kabwe, Albert Msando akiwasili Mahakama Kuu kusikiliza hukumu ya Zitto.


Mwanasheria wa Chadema, Peter Kibatara (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa chama hicho, Tundu Lissu ndani ya Mahakama Kuu tayari kusikiliza hukumu ya Zitto.…


Tundu Lissu akitoka mahakamani baada ya chama chake kushindwa na Zitto.


Aidha Wakili wa chama cha CHADEMA,Tundu Lisu ameeleza kutoridhika na maamuziki ya Mahakama,hivyo akabanisha kuwa  Zitto Kabwe atabaki kuwa Mbunge wa Mahakama,na kama tujuavyo Mbunge wa Mahakama una  muda wake basi tujipe muda tuu..alibainisha Tundu Lisu.



Albert Msando akiongea na wanahabari baada ya kushinda hukumu hiyo.


Baadhi ya mabango waliyokuwa nayo wananchi.




Ulinzi mkali nje ya Mahakama Kuu.



Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Bw. Zitto Zuberi Kabwe amekigalagaza chama chake baada ya kuibuka mshindi katika hukumu iliyosomwa na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, John Utamwa.

Hukumu hiyo imetolewa leo(Januari 07,2014) majira ya saa 11 jioni baada ya Zitto kuwasilisha shauri la kuiomba mahakama iweke zuio kwa Kamati Kuu ya Chadema (CC) kumjadili kuhusu uanachama wake.

Mahakama Kuu imeamua Zitto aendelee kuwa mwanachama hai wa Chadema mpaka itakamalizika kesi ya awali aliyofungua akidai Chadema kumrejeshea nyazifa zake zote alizovuliwa na chama hicho na kwa kipindi hiki haki zote za mbunge huyo zitakuwa chini ya uangalizi wa mahakama mpaka kesi itakapomalizika na kutolewa hukumu.

Zitto alifungua kesi ya kudai kurejeshewa nyazifa zake ambazo alivuliwa mwishoni mwa mwaka jana, kesi hiyo iliambatana na kesi nyingine aliyoifungua hivi karibuni akiomba Kamati kuu isijadili kuhusu uanachama wake mpaka itakapoisha kesi yake ya awali.

Kesi ya awali ya mbunge huyo kudai kurejeshewa nyazifa zake itaunguruma tena Februari 13, mwaka huu.


Aidha Wakili wa chama cha CHADEMA,Tundu Lisu ameeleza kutoridhika na maamuziki ya Mahakama,hivyo akabanisha kuwa  Zitto Kabwe atabaki kuwa Mbunge wa Mahakama,na kama tujuavyo Mbunge wa Mahakama una  muda wake basi tujipe muda tuu..alibainisha Tundu Lisu.
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad