Taswira ya Vurugu mahakamani zilizohusisha wafuasi wa Chadema wanaomuunga mkono Zitto na wale wanaompinga. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, January 04, 2014

Taswira ya Vurugu mahakamani zilizohusisha wafuasi wa Chadema wanaomuunga mkono Zitto na wale wanaompinga.

Wanachama wa Chadema, wakitwangana nje ya Mahakama Kuu, jijini Dar es Salaam na Vurugu hizo zilihusisha wafuasi wa chama hicho wanaomuunga mkono Zitto na wale wanaompinga, ambao walikuwa wamebeba mabango ya kumsifia na wengine wakiwa wamebeba ya kumkashifu.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa, akimwelekeza jambo Katibu Mwenezi wa chama hicho John Mnyika, wakati wa kikao cha Kamati Kuu, kilichofanyika  Dar es Salaam jana. Kulia ni Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe.


Mwanachama wa Chadema, anayepinga hoja za Zitto Kabwe, akimtwanga mfuasi wa Zitto Kabwe.

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeahirisha kutoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa jana na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zuberi Kabwe (Chadema), kuhusu ombi la kuitaka Mahakama hiyo kuizuia Kamati Kuu ya Chama hicho, kutomjadili katika kikao ambacho kilipangwa kufanyika leo jijini Dar es Salaam.

Jaji John Utumwa alisitisha kutoa hukumu hiyo mpaka siku ya Jumatatu (Januari 06,2014)saa 4:00 asubuhi.

Hata hiyo baada ya Jaji huyo kuahirisha kesi hiyo, nje ya Mahakama hiyo kulikuwa na vurugu kubwa baada ya kundi linalo unga mkono maamuzi ya Chadema kutwangana na kundi linalo muunga Zitto Kabwe.

Hatua hiyo ilisababisha Askari wa Jeshi la Polisi kuingilia kati, huku wakiungana na upande wa Chadema na kuwatwanga marundi wafuasi wa Zitto waliokuwa na mambango kama ilivyokuwa kwa wenzao wa Chadema.

Kesi hiyo ilifunguliwa jana na wakili wa Mbunge huyo Albert Msando huku wakili wa Chadema Tundu Lissu akiweka pingamizi,hata hivyo Jaji John Utumwa wa Mahakama hiyo alitupilia mbali mapingamizi yote yaliyowekwa na Tundu Lissu.

Mara baada ya kuwasili kwa Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini, huku akiwa ameongozana watu kadhaa wakiwamo wanasheria wake na mabaunsa, wanachama hao walianza kumzomea huku baadhi wakimwita fisadi.

Hali hiyo iliibua zogo katika eneo la mahakama hiyo, hali iliyowalazimu maofisa kadhaa wa polisi kuingilia kati kwa kuamua kumchukua Zitto na kumhifadhi kwenye chumba maalumu na kumtoa saa 6 mchana kesi yake ilipoanza kusikilizwa.  

Baadhi ya mabango ya kumkashifu  yalisomeka; Zitto tulimpenda, CCM imempenda zaidi, Zitto rudisha fedha za CCM.

Yale yaliyomsifia yalisomeka; Zitto kama Mandela na Zitto ni Mkombozi.

Baada ya kumalizika kusikilizwa kwa kesi hiyo, saa 12 jioni wanachama hao walianza kurushiana ngumi, hasa baada ya kuibuliwa kwa mabango yaliyosomeka ‘Zitto kwanza Chadema baadaye’.

Zitto aliomba  Mahakama hiyo kuzuia Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema  kumjadili hadi rufaa yake aliyoikata kwenye Baraza Kuu  la Chadema  itakaposikilizwa na kuamuliwa na wazuiwe kumwingilia katika utekelezaji wa majukumu yake ya ubunge wa Kigoma Kaskazini .

Pia aliiomba Mahakama hiyo Kuu kumwamuru  Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa  ampatie nakala ya mashtaka na maelezo ya uamuzi uliofikiwa na  Kamati Kuu  Novemba 22, 2013 na kusababisha avuliwe nyadhifa zake ili aweze kupeleka rufaa yake Baraza Kuu la Chadema kupinga uamuzi huo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad