Mabeki wa
KCC walimdhibiti vizuri winga machachari wa Simba SC, Ramadhani Yahya Singano
‘Messi’ wakati pia beki Mkenya, Donald
Mosoti Omwanwa aliiongoza vyema safu ya ulinzi ya Simba SC.
Matokeo hayo
yanazifanya Simba SC na KCC ziendelee kukabana kileleni, kila timu ikiwa na
pointi nne baada ya kucheza mechi mbili.
Mapema jioni
katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo, wenyeji KMKM nao walitoshana nguvu na
AFC Leopard ya Kenya kwa sare ya 0-0 pia.
Mechi za
Kundi B zitahitimishwa Januari 5, kwa Simba kumenyana na KMKM na KCC na
Leopard.
Michuano
hiyo itaendelea leo(Januari 04,2014) kwa mechi za Kundi C, Ashanti ikimenyana
na Spice Stars na Azam FC na Tusker ya Kenya Uwanja wa Amaan, wakati Uwanja wa
Gombani, Pemba Clove Stars itamenyana na URA ya Uganda na Mbeya City na Chuoni.






No comments:
Post a Comment