SOMA:-Taarifa ya (CAG) Utoh ili kutatua mgogoro uliokuwepo katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera na Meya wake Bw.Anatory Amani kujiuzulu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, January 18, 2014

SOMA:-Taarifa ya (CAG) Utoh ili kutatua mgogoro uliokuwepo katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera na Meya wake Bw.Anatory Amani kujiuzulu.

Kutoka kushoto: Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Nassor Mnambila, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh. Fabian Massawe, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh wakiingia ukumbini mjini Bukoba….ambapo… MEYA wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani amejiuzulu wakati Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Khamis Kaputa na wakuu wa idara tatu ambao ni Mhandisi Nimzihilwa, Ofisa Ugavi Baraka Marwa na Mweka Hazina Ulomi wakivuliwa uongozi baada ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyosomwa Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.


Viongozi hao wakifungua kikao hicho cha kusomwa ripoti ya ukaguzi maalum ya CAG  Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Nassor Mnambila akifungua kikao.…hicho cha kusomwa ripoti ya ukaguzi maalum ya CAG  Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh. Fabian Massawe akimkaribisha mgeni rasmi kwenye kikao hicho cha kukamilisha Ukaguzi Maalum " Exit Meeting" cha CAG.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh akisoma ripoti ya ukaguzi maalum Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.

Baadhi ya waliohudhuria kikao hicho cha kusomwa ripoti ya ukaguzi maalum Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.

Baadhi ya waliohudhuria kikao hicho cha kusomwa ripoti ya ukaguzi maalum Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.

Meya wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani (kulia) pamoja na Madiwani wa Manispaa ya Bukoba katika kikao hicho.

Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri (kulia) na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh (kushoto) wakiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Bw. Fabian Massawe (kati) katika meza kuu Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.

Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri (katikati) akimsikiliza kwa makini Bw. Ludovick Utouh.

Viongozi meza kuu wote walikuwa makini  kusikiliza taarifa hiyo ya Ukaguzi iliyosomwa jana na CAG Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.

Taswira ya kikao hicho katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa Jana (Januari 17,2014) katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Kagera kutatua mgogoro uliokuwepo katika manispaa hiyo.

Madiwani wa Manispaa ya Bukoba pamoja na Mstahiki Meya Anatory Amani ambaye madiwani wa manispaa wanamtuhumu kwa matumizi mabaya ya madaraka. (PICHA KWA HISANI YA BUKOBA SPORTS BLOG)


Taarifa ya (CAG) Utoh.

Waziri mkuu alituomba tufanye ukaguzi maalum,
Mwaka 2013 tulifika bukoba na kufanya kikao cha kwanza na wadau.
Katika kikao hicho nilitoa maombi ambayo mliyafuata nawashukuru,madiwani na wananchi walitusaidia saana.

Natoa taadhari kwamba tulikuwa na baadhi za rejea ambazo ndizo tulizofuata,tulipokea maombi ya wananchi wengi lakini hayakuwepo katika rejea,hatukuyafanyia kazi  , Kilichobainika,Tunapohitaji maendeleo,tunafanya vitu kwa nia njema bila kufuata taratibu

Kuhusu uwekezaji wenye mashaka kwenye kituo cha kuosha magari,zabuni haikuwa shindanishi ni kiyume na taratibu cha taribu anataja kifungu kilichokiukwa

Waliosaini ni Khamis kaputa na anatory amani huku wakijua ilikuwa ni makosa kufanya hivyo bila idhini ya kikao cha madiwani,pia kampuni husika ya ASEC ilikuwa haijasajiliwa na BRELA. hailipi kodi TRA

2.Issue ya Viwanja.

Kati ya wananchi 800 waliotakiwa kugawiwa viwanja ni 300 waliogawawia kutokana na migogoro ya viwanja kimila.

Manispaa ilingia makubaliano na UTT kupima viwanja elfu 5 kwa kugawana faida ya asilimia 50 kwa 50 baina ya UTT manispaa ilisainiwa na kaimu meya ngalinda bila kupata idhini ya baraza la madiwani

Pia walikopa fedha kutoka UTT bila kupata ridhaa ya waziri mwenye thamana.

3.Issue ya matengenzo ya barabara mpya.

Manispaa ya bukoba iliingia mkataba na mkandarsai aitwaye KAJUNA INVESTMENT mkataba ulikuwa wa sh 138 milioni alilipwa fedha za dharula ambazo hazikuwa na nyaraka hivyo malipo ya mkandarasi huyu yaliongezwa hadi kufikia sh sh 227 kwa kutumia barua iliyosainwa na tofauti na hali ya awali.haikuwapa idhini ya mkandarasi wa serikali na kinyume na kanuni za manunuzi ya umma.anasoma kifungu kilichokiukwa

4.issue ya Ujenzi wa soku kuu.

Utaratibu wa kutaka kujenga soko kuu la bukoba haikupata idhini ya madiwani ya kumlipa mkandarasi mshauri OGM milioni 789 huku pia akawaita madiwani na kuwaeleza kuwa mkandarasi anahitaji jumla la miliini 590 milioni. Mmojawapo wa madiwani mh lunagisa alikataa pale pale kwenye kikao.

5.Issue ya kuhamisha wafanyabisha wa Bukoba.

Mh Meya anatory aman aliomba mkopo kwa kazi hiyo bila kibali cha madiwani na mawaziri.mkopo huo hata hivyo haukupatika.

6.Mkandaasi wa OGM.

Hakuwa kwenye orodha ya walioomba zabuni ya kufanya kazi ya ukandarasi ushauri wa kufanya kazi katika ujenzi wa soko kuu lakini alionekana kwenye rodha baadaye ya waliolipwa .Wakandarasi wote waliolipwa fedha hizo walikuwa hawalipi kodi TRA-hivyo TRA ina haki ya kuwadai hizo kodi.

7.Ujenzi wa stendi kuu ya Bukoba.

Mradi huu hakutengezwa kwenye gazeti la serikali lakini walipata mkandarasi na kumlipa fedha za kazi hiyo kinyume na taratibu za serikali.

Gazeti lilotangaza tenda hiyo halikupatikana.pia timu ya ukaguzi ilitembelea eneo la kazi na kubaini kuwa mkandarasi alilipwa fedha nyingi tofauti na kazi aliyoifanya

9.Mradi wa maji.

Kila kata iliyopangwa kuwekwa mradi wa maji ilitakiwa kuchangia asilimia 2 hivyo kata anakotoka meya ilitimiza kigezo na kupata huduma hiyo.

fedha za kata zilitolewa na meya kwa kata yake.hivyo kitendo cha kata ya meya kupata huduma hakuwa na tatizo.Tuhuma hizi kuwa meya alitoa huduma kwa kata yake ni uongo.

10.Issue ya uuzwaji viwanja vya wazi.

Mkataba wa kununua kiwanja kinacholalamikiwa hakufuata taratibu za ununuzi
Ni katika bweni la sekondari ya PEACE inayomilikiwa na Meya.

Tunapendekeza kuundwa kwa timu maalumu kuchunguza tuhuma hizi kwani katika eneo hili hatukufikia mwisho

11.Ujenzi wa barabara:- kwa lami kwenye kata ya meya toafuti na fedha zilizoombwa.

Manispaa iliomba milioni 30 kukarabati barabara hiyo lakini TAMISEMI ilitoa milioni 300 na walihoji TAMISEMI walisema hilo ni la kawaida hivyo tuhuma hizo ni UONGO

12.Mradi wa Ujenzi wa Bwawa.

Hakuwahi kujadiliwa na baraza la madiwani,ulikuwa ni mradi wa wajanja tu

13.Issue ya wafanyabishara soko kuu kutolipa kodi.

Manispaa Imekosa mapato sh milioni 256 zimepotea kutokana na chanzo hicho cha wafanyabishara wa soko kuu kutolipa kodi kutokana na mgogoro unaondelea

14.Issue ya matumizi ya gari Sm 4663.

Gari hili limekuwa likiegeshwa kwa ofisi ya redio kasibante ya kagasheki.

Kumbukumbu za TRA zinaonesha kuwa ni mali ya halmashauri lakini alipohojiwa Kagasheki alidai kuwa alinunua kwa fedha zake. 

Lakini halmashauri haina kumbukumbu zozote juu ya gari hilo

Tunapendekeza lilerejeshwe kwenye halmshauri kama ataona ni manufaa kwa wananchi lakini kama haitawezekana basi gari hilo libadilishiwe usajili ili lionekane ni la kiraia

15.Uteuzi wa wakala wenye upendeleo kwenye ushuru wa basi.

Zabuni ya aliyepata rufaa ilitenguliwa kwani haikuwa imesajiliwa na mamlaka husika
Alibadilisha jina na kuomba tena kisha kupata,muombaji aliyeomba kwa tozo ya juu alinyimwa.

Manispaa ilifanya upendeleo na kukosa sh million 46 kwa mwaka

16:Issue ya posho kwa madiwani katika safari ya mafunzo nje ya wilaya.

Madiwani wawili walitakiwa kulipwa sh laki 4 kila mmoja kwa safari hawakusafiri lakini fedha hizo hazikurudishwa kwa manispaa na kukatiwa risiti,.hazionekani zilipo

17.Issue ya vibanda vya maduka.

Ukaguzi hakudhibitisha kuwepo tatizo la katika dai hili kwani nyaraka zinaonesha kutokuwepo tatizo.bali inashauri kuwepo kwa mkanganyiko na wapangaji wake

18.Issue ya deni katika uwanja wa mpira kaitaba.

Uwanja ulikarabatiwa na kiwanda cha sukari kagera kwa madai ya kurejeshewa fedha zake.sehemu ya fedha hazijarudishwa.Tume inapendekeza kufanya muafaka na kiwanda au itafute fedha za kulipa deni

19.Kutowajibika ipasavyo kwa ukaguzi wa ndani.

Kipo kwa ajili ya kushauri na kuziba mianya ya matumizi mabaya ya fedha.

Aliyekuwepo amehojiwa juu ya miradi hiyo na kwamba halikuwa hajui lolote na hakuweza kumshauri mkurugenzi ipasavyo

20.Mteuzi katika bodi ya maji.upendeleo kwa mmoja wa madiwani.

Waziri mwenye thamana aliteuwa
 
Hitimisho.

Hatukuweka chumvi,tuliyosema ndiyo ukweli tupu.

Namshukuru waziri mkuu kwa kunipa kazi hii ya kukaguzi katika manispaa

Utaratibu wa uwasilisahji wa ripoti maalum tutaipeleka kwa aliyeomba ukaguzi huu.
ASANTENI


Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri  akiongea kwa niaba ya Waziri mkuu alitoa taarifa hii kama ifuatavyo



Maelekezo ya waziri mkuu.

Makosa ya meya Anatory kufanya makubaliano bila idhini ya madiwani na taratibu za serikali basi ajipime mwenyewe na kujiuzuru kwa maslahi ya manispaa ya bukoba.

Akikataa basi madiwani wamuondoe

Watumishi wa manispaa wachukuliwe hatua

Bw Khamis kaputa avuliwe madaraka.

Mhandisi,mweka hazina nk wapoteze vyeo vyao

Wakandarasi wote waliopata fedha bila taratibu wazirejeshwe.

Alipopewa nafasi, Meya ametangaza kujiuzulu rasmi nafasi yake

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad