 |
MBALI na
kipigo cha mabao 4-0 kutoka Liverpool usiku huu, Everton ilipata pigo lingine
baada ya mshambuliaji wake tegemeo, Romelu Lukaku kutolewa nje kwenye machela
katika mechi hiyo ya mahasimu wa Merseyside baada ya kuumia.
Mshambuliaji
huyo wa mkopo kutoka Chelsea, aliumia kifundo cha mguu baada ya kuangukiwa na
mchezaji mwenzake Gareth Barry akijaribu kumzuia bila mafanikio Steven Gerrard
kufunga bao la kwanza.
Nafasi ya
Lukaku ilichukuliwa na Steven Naismith dakika ya 25 tu ya mchezo huo Uwanja wa
Anfield.
|
 |
Mshambuliaji
huyo wa Ubelgiji akitolewa nje kwa machela baada ya kuumia na kushindwa kuendelea
na mchezo, Romelu Lukaku aliumia baada
ya kuangukiwa na Gareth Barry
|

 |
Nyota wa
Southampton, Adam Lallana, katikati, akishangilia baada ya kuifungia timu yake
bao la kusawazisha dhidi ya Arsenal ambapo bao la Adam Lallana limeosha kuipa
sare ya 2-2 Southampton katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya vinara,
Arsenal ambao sasa wanawafungulia milango Manchester City na Chelsea kwenye
mbio za ubingwa.
Nyota huyo
wa kimataifa wa England alifunga kiasi cha dakika mbili baada ya Santi Cazorla
kuifungia Arsenal dakika ya 52 na kumuachia presha kocha Arsene Wenger katika
kampeni za ubingwa.
Southampton
ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Jose Fonte dakika ya 21, lakini Oliver
Giroud akaisawazishia The Gunners dakika ya 48. Arsenal walimaliza mechi wakiwa
10 baada ya Mathieu Flamini kuonyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja.
Arsenal sasa
inakuwa na pointi 52 baada ya kucheza mechi 23, ikifuatiwa na Manchester City
yenye pointi 50 na Chelsea pointi 49, ingawa zote zimecheza mechi 22.
|
 |
Kiungo wa
Arsenal, Santi Cazorla, katikati, akishangilia na wenzake baada ya kufunga bao
la pili na kutoka sare ya 2-2 na
Southampton katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya vinara, Arsenal ambao
sasa wanawafungulia milango Manchester City na Chelsea kwenye mbio za ubingwa.
|
 |
Mchezaji
ghali kwenye historia ya klabu ya Man Utd Juan Mata alivaa jezi yake namba 8 ya
Man United baada ya kutengeneza bao la kwanza la timu hiyo lililofungwa na
Robin van Persie katika ushindi wa 2-0 dhidi ya cardiff City Uwanja wa Old
Trafford jana (Januari 28,2014) usiku huu.
|
 |
Robin van
Persie akipongezwa na wenzake baada ya kufunga bao la kwanza akirejea kutoka
kwenye majeruhi Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya England, ilibidi kocha David
Moyes asuburi hadi dakika ya 59 kujihakikishia ushindi kwa bao zuri la shley
Young.
Matokeo hayo
yanaifanya United itimize pointi 40 baada ya kucheza mechi 23, ikibaki nafasi
ya saba.
|
RATIBA YA MECHI ZA LEO EPL 2013 / 2014 JANUARI 29,2014.
No comments:
Post a Comment