Afariki baada ya kuanguka kutoka jengo la makao makuu ya benki ya JP Morgan mjini London nchini Uingereza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, January 28, 2014

Afariki baada ya kuanguka kutoka jengo la makao makuu ya benki ya JP Morgan mjini London nchini Uingereza.

Sehemu ya juu ya jengo la benki ya PJ Morgan (iliyozungushiwa mduara mwekundu) ambayo mtu huyo anasemekana alijirusha na kuangukia sehemu ya chini (yenye mduara) na kufa.


Eneo la jumla la sehemu lilipotokea tukio hilo. (Picha: David Price) ambapo Polisi walisema walimkuta mtu huyo katika ghorofa ya tisa na kwakmba  wanayafahamu maelezo yake lakini  wanasubiri utambulisho zaidi.


Mtu mmoja mwenye umri wa miaka 39, amefariki leo(Januari 28,2014) asubuhi majira ya saa mbili baada ya kuanguka kutoka jengo la makao makuu ya benki  ya JP Morgan mjini London, Uingereza,  eneo la Canary Wharf.

Inasemekana mtu huyo alijirusha kutoka sehemu ya juu ya jengo hilo na kuanguka katika sehemu ya juu iliyotokeza mbele ya jengo hilohilo kabla ya kufika chini.

Polisi walisema walimkuta mtu huyo katika ghorofa ya tisa ambapo wanayafahamu maelezo yake lakini  wanasubiri utambulisho zaidi, na kwamba hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo hadi sasa na kwamba uchunguzi unaendelea.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad