Hili ndio Taswira ya basi la Kampuni ya Mtei lilivyochomwa moto na Wananchi mkoani Singida likiwa safarini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, January 10, 2014

Hili ndio Taswira ya basi la Kampuni ya Mtei lilivyochomwa moto na Wananchi mkoani Singida likiwa safarini.

Basi la kampuni ya Mtei lenye T 742 ACU Scania likiwa limeteketezwa kwa moto na wananchi baada ya kugonga na kusababisha vifo vya watu watatu wa familia moja mjini Singida jana(Januari 09,2014).


Tukio hilo lilitokea jana (Januari 09,2014) saa 1:10 asubuhi katika eneo la Ijanuka, nje kidogo ya mji wa Singida…Lilitokea kufuatia dereva wa basi la Mtei lenye namba za usajili T 742 ACU aina ya Scania, Dismas Ludovick, akijaribu kuipita pikipiki yenye namba za usajili T 368 BXZ ikiwa na abiria watatu na dereva wao.


Abiria wanasema  walipokusanyana wananchi, walitafuta mafuta ya petroli na kumwaga ndani ya basi hilo kisha wakalipua kibiriti.


Wananchi wenye hasira, jana walifanya kitendo cha kikatili kwa kulichoma moto basi la kampuni ya Mtei lililokuwa likisafiri kutoka Singida kwenda Arusha, baada ya kugonga bobaboda na kuua watatu wa familia moja.

Tukio hilo lilitokea jana (Januari 09,2014) saa 1:10 asubuhi katika eneo la Ijanuka, nje kidogo ya mji wa Singida…na Lilitokea kufuatia dereva wa basi la Mtei lenye namba za usajili T 742 ACU aina ya Scania, Dismas Ludovick, akijaribu kuipita pikipiki yenye namba za usajili T 368 BXZ ikiwa na abiria watatu na dereva wao.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, alisema baada ya pikipiki hiyo kugongwa na basi hilo lililokuwa na abiria tisa, watu wawili waliokuwa wamepakiwa walifariki dunia papo hapo na mwingine mmoja kufia Hospitali ya Mkoa wa Singida.

Aliwataja waliofariki dunia kwa jina moja moja kuwa ni Tamili, Kassim na Hamza, wote watoto wa mmiliki wa pikipiki hiyo, Shabani Bunku, mkazi wa Ijanuka, ambaye naye yupo mahututi na amelazwa katika hospitali hiyo.

Kwa mujibu wa baadhi ya wananchi waliofika eneo la tukio, marehemu hao walikuwa wanakwenda shambani na baba yao.

Kamanda Kamwela alisema wakati dereva wa basi anajaribu kuipita, pikipiki hiyo, nayo ilikata kona kuelekea kulia, hali iliyosababisha kukanyagwa na kuburuzwa mita 20 kutoka eneo la tukio.

Mashuhuda wa tukio hilo, akiwamo Husna Ramadhani, Yassin Ibrahim na Samuel Massawe, waliokuwa kwenye basi la Mtei, walisema kuwa baada ya pikipiki kugongwa, wananchi wa eneo hilo waliwasiliana kwa simu na kukusanyika kwa haraka.

Walisema walipokusanyana, walitafuta mafuta ya petroli na kumwaga ndani ya basi hilo kisha wakalipua kibiriti.

Mashuhuda hao walisema kuwa kabla wananchi hao kuchukua hatua hiyo, walivunja kwanza vioo vyote vya madirisha ya basi hilo.

“Walianza kukusanyika kidogo kidogo huku wakipigiana simu, walipojaa walianza kuvunja vioo vyote vya madirisha huku wakidai kwamba mabasi ya Mtei yamezidi sana kuwakanyaga pamoja na ng’ombe wao, leo acha na yeye wamkomeshe,” alidai mmoja wa abiria wa basi hilo.

Husna, abiria aliyekuwa anasafiri kwenda Arusha, alisema alipata hasara katika sakata hilo kwa kuwa alipoteza begi la nguo lililoteketea kwa moto pamoja na mfuko wa nyanya alizokuwa anapeleka kama zawadi kwa ndugu zake.

Kamanda Kamwela aliwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi na ameahidi kuwasaka wote wakiwamo vinara wa tukio hilo la uchomaji moto basi hilo ili wafikishwe kwenye vyombo vya sheria. 

Habari Na:-Nipashe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad