Aliyekuwa waziri Mkuu wa Israel, Ariel Sharon amefariki dunia leo Januari 11, 2014 akiwa na umri wa miaka 85. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, January 11, 2014

Aliyekuwa waziri Mkuu wa Israel, Ariel Sharon amefariki dunia leo Januari 11, 2014 akiwa na umri wa miaka 85.

Waziri Mkuu wa zamani wa Israel, Ariel Sharon enzi za uhai wake….Alikuwa katika hali ya umahututi kwa miaka nane tangu mwaka 2006.



Waziri Mkuu wa zamani wa Israel, Ariel Sharon amefariki dunia leo Januari 11, 2014 akiwa na umri wa miaka 85.

Sharon, aliyekuwa Waziri Mkuu wa 11 wa taifa hilo la kiyahudi, alikuwa kiongozi wa chama cha Likud, lakini katika mzozo mkubwa ndani ya chama hicho kufuatia tofauti za kimtizamo kuhusu ukanda wa Gaza, alijitoa Novemba 2005 na kuanzisha chama chake cha Kadima akiwa bado madarakani.

Alitegemewa kushinda katika uchaguzi uliotarajiwa kufanyika baadaye, lakini ghafla Januari 4 mwaka 2006 alipata ugonjwa wa kupooza mwili mzima na alibakia katika hali hiyo mbaya kwa muda wa miaka nane hadi alipofariki leo Januari 11, 2014.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad