|
|
Baada ya
kupata bao la kwanza, Coastal ilizidi kuwa bora na kuipa Yanga wakati mgumu
zaidi.
Bao la pili
lilipatikana katika dakika ya 88 huku Yanga wakiamini walikuwa wanakaribia
kusawazisha.
Nao Azam FC
imefanikiwa kushika nafasi ya tatu katika michuano ya vijana chini ya umri wa
miaka 20 kwa klabu za Ligi Kuu ya Bara, maarufu kama Kombe la Uhai, baada ya
kuifunga kwa penalti 3-1 Mtibwa Sugar kufuatia sare ya 3-3 ndani ya dakika 120
Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Dakika 90 za mchezo huo zilimalizika timu hizo zikiwa zimefungana mabao 2-2 na zilipoongezwa dakika 30 kila timu ikapata bao moja zaidi.
Mabao ya Azam yalifungwa na Eric Haule dakika ya 32, Adam Omary dakika ya 38 na Ahmed Abbas dakika ya 109, wakati mabao ya Mtibwa yalifungwa na Ally Makarani dakika ya 16, Hassan Mbande dakika ya 81 na Issa Kiganga kwa penalty dakika ya 105.
Penalti za Azam zilifungwa na Mgaya Abdul, Shiraz Abdallah na Ahmed Abbas, wakati ya Mtibwa ilifungwa na Jumanne Mlindwa.





No comments:
Post a Comment