Bao pekee la
Haroun Athumani Chanongo dakika ya 57 limetosha kuipa Tanzania Bara,
Kilimanjaro Stars ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Somalia mchana wa leo(Desemba 01,2013)
katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA
Challenge Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
Kwa matokeo
hayo, Stars imetimiza pointi nne baada ya awali kutoa sare ya 1-1 na Zambia
katika mchezo wake wa kwanza na mustakabali wake wa kuingia Robo Fainali
utategemea matokeo ya mechi za mwisho za kundi hilo.
Katika mchezo
wa leo, Stars ilikuwa inaanza vizuri kutokea nyuma, lakini wanapofika kwenye
eneo la wapinzani wanaharibu, ama kwa kupeana pasi mbovu au kupokonywa mipira
kirahisi.
Na hakukuwa
na uelewano kabisa baina ya washambuliaji wa Stars, Elias Maguri, Amri Kiemba
na Mrisho Ngassa hali ambayo ilifanya mabeki wa Somalia wacheze kwa uhuru
zaidi.
Somalia
walicheza vizuri kipindi cha kwanza na kukosa mabao mawili ya wazi, kutokana na
juhudi za kipa Ivo Mapunda kuokoa hatari zote.
Kipindi cha
pili, kocha Mdenmark Kim Poulsen alianza na mabadiliko, akiwatoa Kiemba na
Maguri na kuwaingiza washambuliaji wawili a Simba SC, Ramadhani Singano na
Haroun Chanongo ambao walibadilisha mchezo.
Pasi nzuri
ya Singano ‘Messi’ iliunganishwa nyavuni na Chanongo dakika ya 57 kuipatia
Stars bao hilo pekee.
Baada ya bao
hilo, Stars iliendelea kushambulia kupitia kwa Singano na Chanongo, lakini
wakaishia kukosa mabao ya wazi. Somalia nayo iliendelea kushambulia lango la
Stars na kuishia kukosa mabao mawili ya wazi, sifa zimuendee Ivo Mapunda.
Kim Poulsen
alimtoa Mrisho Ngassa dakika ya 79 na kumuingiza Farid Mussa, lakini mabadiliko
hayo hayakuleta jipya upande wa Stars.
Kikosi cha
Stars leo kilikuwa; Ivo Mapunda, Himid Mao, Erasto Nyoni, Said Morad, Kevin
Yondan, Frank Domayo, Salum Abubakar, Athumani Iddi ‘Chuji’, Elias
Maguri/Haroun Chanongo dk46, Amri Kiemba/Ramadhani Singano ‘Messi’ dk46 na
Mrisho Ngassa/Farid Mussa dk79.
Somalia;
Mohamed Sherif, Hassan Ali Roble, Mohammed Tahlil Shidane, Aden Hussein
Ibrahim, Hassan Hussein Mohamed, Daud Abdullah Hassan, Sidi Mohamed Omer,
Mohamed Abdi Hayow/Mahmoud Adi Mohamed dk63, Jabril Hassan Mohamed, Mohamed
saleh Hussein na Sadaq Abdulkadir Mohamed/Deki Abdullah Nur dk88.
MAKUNDI 2013/2014.
|
Kundi A |
KUNDI B |
KUNDI C |
|
-Kenya -Ethiopia -Zanzibar -South Sudan |
-Tanzania Bara -Zambia -Burundi -Somalia |
-Uganda -Rwanda -Sudan -Eritrea |
**FAHAMU: Timu mbili za Juu kila Kundi zitasonga Robo Fainali pamoja na Washindi wa Tatu wawili Bora.
RATIBA/MATOKEO.
|
TAREHE |
NA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
SAA |
|
Jumatano Novemba 27 |
1 |
Zanzibar 2 South Sudan 1 |
A |
Nyayo |
1400 |
|
2 |
Kenya 0 Ethiopia 0 |
A |
Nyayo |
1630 |
|
|
Alhamisi Novemba 28 |
3 |
Burundi 2 Somalia 0 |
B |
Machakos |
1400 |
|
4 |
Kili Stars 1 Zambia 1 |
B |
Machakos |
1600 |
|
|
Ijumaa Novemba 29 |
5 |
Sudan 3 Eritrea 0 |
C |
Machakos |
1400 |
|
6 |
Uganda 1 Rwanda 0 |
C |
Machakos |
1600 |
|
|
Jumamosi Novemba 30 |
7 |
Ethiopia 3 Zanzibar 1 |
A |
Nyayo |
1400 |
|
8 |
South Sudan 1 Kenya 3 |
A |
Nyayo |
1600 |
|
|
Jumapili Desemba 1 |
9 |
Somalia 0 v 1 Kili Stars |
B |
Nyayo |
1400 |
|
10 |
Zambia v Burundi |
B |
Nyayo |
1600 |
|
|
Jumatatu Desemba 2 |
11 |
Sudan v Rwanda |
C |
Machakos |
1400 |
|
12 |
Eritrea v Uganda |
C |
Machakos |
1600 |
|
|
Jumanne Desemba 3 |
13 |
South Sudan v Ethiopia |
A |
Machakos |
1400 |
|
14 |
Kenya v Zanzibar |
A |
Machakos |
1600 |
|
|
Jumatano Desemba 4 |
15 |
Kili Stars v Burundi |
B |
Nyayo |
1400 |
|
16 |
Somalia v Zambia |
B |
Nyayo |
1600 |
|
|
Alhamisi Desemba 5 |
17 |
Rwanda v Eritrea |
C |
Nyayo |
1400 |
|
18 |
Uganda v Sudan |
C |
Nyayo |
1600 |
|
|
Ijumaa Desemba 6 |
MAPUMZIKO |
||||
|
ROBO FAINALI |
|||||
|
Jumamosi Desemba 7 |
19 |
C1 v B2 |
Mombasa |
BADO |
|
|
20 |
A1 v 3 BORA 1 |
Mombasa |
BADO |
||
|
Jumapili Desemba 8 |
21 |
B1 v 3 BORA 2 |
Mombasa |
BADO |
|
|
22 |
A2 v C2 |
Mombasa |
BADO |
||
|
Jumatatu Desemba 9 |
MAPUMZIKO |
||||
|
Jumanne Desemba 10 |
NUSU FAINALI |
||||
|
23 |
Mshindi 19 v Mshindi 20 |
BADO |
|||
|
24 |
Mshindi 21 v Mshindi 22 |
BADO |
|||
|
Desemba 11 |
MAPUMZIKO |
||||
|
Alhamisi Desemba 12 |
25 |
Mshindi wa Tatu |
1400 |
||
|
26 |
FAINALI |
1600 |







No comments:
Post a Comment