Na. Aron Msigwa – MAELEZO,Dar es salaam.
Uwezo wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi
nchini kwa mwaka 2011/2012 unaonyesha kuongezeka kutokana na
maboresho mbalimbali yaliyofanyika katika sekta ya elimu,
afya, umiliki wa biashara, shughuli za kilimo, umiliki wa Vifaa na Rasilimali ,
makazi bora, ongezeko la shughuli za kiuchumi na ajira.
Amesema kuwa utafiti huo ulifanyika kuanzia
mwezi Oktoba 2011 hadi Oktoba 2012 ambapo jumla ya kaya 10,186 kati ya 10,400
zilizokuwa zimelengwa zilihojiwa katika maeneo ya Dar es salaam na maeneo
mengine ya mijini na vijijini kwa Tanzania Bara.
Amesema uchumi wa Tanzania kwa sasa umekua
kutokana na kuimarika kwa sekta za ujenzi, usafirishaji, Elimu, shughuli za
mawasiliano, huduma za afya na huduma za kifedha.
“ Serikali imefanya mambo makubwa na sasa
uchumi wa Tanzania umekua kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa katika
kuboresha miundombinu ,kuwekeza katika sekta ya elimu, usafirishaji,
mawasiliano pamoja na ongezeko la huduma za kifedha” amesema.
Amesema kumekuwa na jitihada mbalimbali
zilizofanywa na serikali zikiwemo kuongeza ujenzi wa shule Zaidi hasa zile za
sekondari ambazo zimewezesha kupanda kwa kiwango cha wanafunzi wanaojiunga
katika elimu ya sekondari kutoka 15% mwaka 2007 hadi asilimia 29% 2011/12.
Amefafanua kuwa idadi ya kaya zinazoishi
katika nyumba zilizojengwa kwa vifaa vya ujenzi vya kisasa, paa za kisasa,
vigae na matumizi ya zege na kuta imara tangu mwaka 2007 imeongezeka kwa 66%.
Ameongeza kuwa matokeo ya utafiti yanaonyesha
kuwa asilimia 4% ya kaya zinamiliki pikipiki, 55% zinamiliki radio na 57% ya
kaya zote angalau mwanakaya mmoja anamiliki simu ya mkononi na kufafanua kuwa
kiasi cha asilimia 78 ya kaya za maeneo ya mengine ya mjini na asilimi 88 ya
kaya za Dar es salaam zinamiliki angalau simu moja ya mkononi.
Katika hatua nyingine Dkt. Servacius
ameeleza wastani wa kiwango cha umasikini wa chakula kitaifa ni asilimia
9.7 na kuongeza kuwa kiwango hicho kinafikia asilimia 11.3 kwa maeneo ya
vijijini huku Dar es salaam ikiwa na kiwango cha chini kabisa cha umasikini wa
chakula kwa asilimia 1.0 na maeneo mengine ya mjini yakiwa na umasikini wa
chakula kwa asilimia 8.7.
Amesema miji mikubwa ina kiwango cha chini cha
umasikini wa chakula kwa asilimia 1.0 ambapo wananchi wanaoishi maeneo mengine
ya mjini wana umasikini wa chakula wa asilimia 8.7.
Ameongeza kuwa umasikini wa mahitaji ya msingi
kwa Tanzania bara ni asilimia 28.2 ikilinganishwa na asilimia 33.3 kwa maeneo
ya vijini na asilimia 21.7 kwa maeneo mengine ya mjini na kubainisha kuwa Dar
es salaam ina kiwango cha chini cha umasikini wa mahitaji ya msingi cha
asilimia 4.1.
Kwa upande wake Afisa Mwandamizi wa Benki ya
Dunia Bw. Richard Martini akitoa salaam za Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia
kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi Bw. Phillipe Dongier, ameipongeza Ofisi
ya Taifa ya Takwimu kwa kuzingatia vigezo vya tafiti vya kimataifa katika
kufuatilia hali ya umasikini na kipato nchini.
Amesema twakimu za utafiti huo zilizotolewa
zinaonyesha hali halisi ya maisha wanayoishi wanachi na kuongeza kuwa
zitaisaidia serikali, wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo kuelewa
na kushiriki kikamilifu katika kuleta maendeleo na kukabiliana na changamoto za
umasikini zilizopo nchini.







No comments:
Post a Comment