Tazama Jambo Bukoba inavyo boresha mazingira ya Shule mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, November 27, 2013

Tazama Jambo Bukoba inavyo boresha mazingira ya Shule mkoani Kagera.

Mwenyekiti wa kijiji cha Kiruruma (mwenye shati la kitenge )  Festo Mtatemba na mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kiruruma Hosea Kagashe (Kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wakati wa makabidhiano ya Chumba cha Darasa.

“Jamii haina budi  kuchangia miradi ya maendeleo katika kupunguza changamoto za miundombinu katika taasisi za serikali ili kuweza kuboresha maisha ya wananchi wanaohitaji taaluma  ndani na  nje ya nchi”…:-Picha / Habari Na:-Shaaban Ndyamukama-Biharamulo.

Wanafunzi wa shule ya msingi Kiruruma wilayani Biharamulo mkoani Kagera wakiwa katika chumba cha darasa kilichojengwa ba Jambo Bukoba kwa kushirikiana na Wananchi wa kijiji .
Mratibu wa Shirika la Jambo Bukoba (aliyechuchumaa) Bw Steven Gonzaga akiwa na wanawake wa kijiji cha Kiruruma wilayani Biharamulo mkoani Kagera ambao ni wajumbe wa serikali ya kijiji na kamati ya shule ya Msingi Kiruruma.
Kutoka Kushoto ni Mr Lucas wa shirika la Jambo Bukoba kutoka nchini Ujerumani akiwa na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kiruruma pamoja na Mratibu wa shirika hilo Bw Steven Gonzaga  wakati wa Makabidhiano ya  chumba cha darasa.
Mmoja wa Wanafunzi akisoma maelezo yanayolenga kuhamasisha  jamii kulitambua Shirika la Jambo Bukoba na kauli mbiu zake za kukuza Vipaji vya Wanafunzi  na Uboreshaji wa Mazingira ya Kujifunzia mkoani  Kagera.


Shirika la Jambo bukoba lililoko mkoani Kagera leo (Novemba 27,2013)   limekabidhi chumba cha darasa chenye thamani ya shilingi milioni 7.9  kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya msingi Kiruruma katika  halmashauri ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.

Mratibu wa shirika hilo Bw Steven Gonzaga amesema kuwa chumba hicho kimejengwa kwa kushirikiana na wananchi ambao wamekusanya vifaa vinavyopatikana katika mazingira yao ambavyo thamani yake ni  zaidi ya 25%.

Bw Gonzaga amesema kuwa shule hiyo imejengewa chumba hicho  baada ya kutaja changamoto ya wanafunzi kusongamana katika darasa moja  wakati  shule hiyo ikishiriki bonanza  la michezo mwaka jana mkoani Kagera.

Katika hatua nyingine amesema kuwa  Shirika  hilo  limetoa msaada wa kujenga baadhi ya miundombinu ya shule tano za msingi  kwenye wilaya kadhaa mkoani humo  kwa lengo la kukuza  vipaji na taaluma kwa wanafunzi wa shule hizo.

Steven Gonzaga amezitaja shule shule hizo kuwa ni Rulenge (Ngara) matundu manne ya vyoo , Tumaini (Bukoba Manispaa) madarasa mawili na ofisi ya walimu  Kalalo (Karagwe) darasa moja  na  Kishoju (Muleba ) iliyotengenezewa  madawati 60. 

Amezitaja shule nyingine kuwa ni Kasambya (Misenyi) ukarabati wa madarasa mawili na ofisi ya walimu, Kiruruma (Biharamulo) ujenzi wa darasa moja na Karwoshe Bukoba ( vijijini ) ukarabati wa madarasa mawili na ofisi ya walimu. 

Hata hivyo Afisa mipango wa halamshauri ya wilaya ya Biharamulo  Zabron Janga kwa niaba ya mkurugenzi wake Nassibu Mbagga  amesema licha ya kupata msaada huo jamii haina budi kuendelea kuchangia  miundombinu  inayokosekana. 

Jamii haina budi  kuchangia miradi ya maendeleo katika kupunguza changamoto za miundombinu katika taasisi za serikali ili kuweza kuboresha maisha ya wananchi wanaohitaji taaluma  ndani na  nje ya nchi”. Alisema Janga

Aliongeza kuwa jamii inategemea sana kupata misaada na kuzidi kuathiri watoto wao katika kupata taaluma kwenye sekta ya elimu  pamoja na miundombinu mingine katika sekta ya afya  Maji na barabara huku ikichtumia gharama kubwa kuchangia anasa kwenye sherehe na harusi mbalimbali.

Shirika la Jambo Bukoba lililoko mkoani Kagera  linasimamiwa na raia wa kitanzania Clemence Mulokozi mzaliwa wa Bukoba anayeishi nchini Ujerumani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad