Ndege ya shirika la Monarch Airlines A321, namba MON 9254, ilipangwa
kutua uwanjani hapo 5.30pm kwa muda wa Ujerumani, lakini rubani
alilazimika kusitisha kutua kwa ndege hiyo kwa sababu kulikuwa na ndege
nyingine kwenye sehemu ya kutulia.
Ndege hiyo waliyopanda United ikabidi izunguke uwanja hewani na kuja
kutua dakika 10 baadae saa 5.40 pm.
Abiria mmoja katika ndege hiyo, ambayo ilikuwa na wachezaji wote wa
United na maofisa wengine wa timu hiyo akiwemo CEO wa zamani wa klabu hiyo
David Gill waliokuwa wakielekea kwenye mchezo wa klabu bingwa ya ulaya dhidi ya
Bayer Leverkusen, alisema kwamba tukio hilo lileta hali ya kutisha miongoni mwa
abiria huku akifhamika kwamba ilitolewa taarifa rasmi kwamba kulikuwa na tatizo
lilokuwa likiendelea.
Mlinzi wa United Rio Ferdinand alitweet kuhusu tukio hilo muda mfupi
baada ya kutua salama akisema, 'Landed in Germany....just....I’ve only just
recovered after that choppy landing!
Kwenye msafara huo hakuwemo Sir Bobby Charlton, mtu mmojawapo
aliyenusurika katika ajali iliyopita ya Munich, pia hakuwemo kocha mstaafu wa
timu hiyo Sir Alex Ferguson.
Pamoja na kuchelewa kutua kwa ndege hiyo huko Cologne, Moyes na mlinzi
Chris Smalling walienda kwenye mkutano wa waandishi wa habari wakiwa watulivu
na wasiokuwa na chembe ya wasiwasi juu ya tukio hilo.
Usiku wa leo (Novemba 27,2013) United inacheza mechi muhimu na
Leverkusen huku wakiwa wana mapengo ya wachezaji wao muhimu kama Van Persie,
Carrick, Jones na Vidic.
MATOKEO YA JANA:-NOVEMBA 26,2013.
Basel 1-0 Chelsea
Steaua Bucuresti 0-0 Schalke 04
Group F
Arsenal 2-0 Marseille
Borussia Dortmund 3-1 Napoli
Group G
Zenit Petersburg 1-1 Atletico Madrid
FC Porto 1-1 Austria Wien
Group H
Ajax 2-1 Barcelona
Celtic 0-3 AC Milan
Sasa Chelsea wametinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA licha ya kufungwa Bao 1-0 na FC Basel hapo
Jana(Novemba 26,2013) huko Uswisi kwenye
Mechi ya Kundi E.
Barcelona walikuwa wameshatinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA
walifungwa Bao 2-1 na Ajax huko Amsterdam na hicho ni kipigo cha kwa kwanza
kwao Msimu huu chini ya Meneja wao mpya Gerardo Martino.
Ajax sasa watasafiri kwenda Italy Mwezi ujao kucheza na AC Milan ambao
Jana waliitandika Celtic 3-0 huko Scotland na Matokeo ya Mechi hii kuamua nani
ataungana na Barcelona.
Katika Kundi F, Timu 3, Arsenal, Napoli na Borussia Dortmund, zina
uwezo wa kupata Nafasi mbili za kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 baada
Arsenal kuifunga Olympique Marseille 2-0 na Borussia Dortmund kuichapa Napoli
3-1.
Arsenal watamaliza Ugenini na Napoli na Dortmund pia wako Ugenini
kucheza na Marseille ambayo imeshaaga Mashindano.
TIMU ZILIZOFUZU KUINGIA Raundi ya Mtoano ya Timu
16:
[Timu 5 Bado 11]
-Bayern Munich
-Manchester City
-Atletico Madrid
-Barcelona
-Chelsea






No comments:
Post a Comment