Taswira ya jengo lililoporomoka eneo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban nchini Afrika Kusini na kuua watu wawili mpaka sasa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, November 20, 2013

Taswira ya jengo lililoporomoka eneo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban nchini Afrika Kusini na kuua watu wawili mpaka sasa.


Watu wawili wamefariki na wengine takriban watu 50 kukwama kwenye vifusi baada ya paa ya jumba la maduka lililokuwa linajengwa kuporomoka nchini Afrika Kusini.




Taswira ya jengo lililoporomoka eneo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban nchini Afrika Kusini na kuua watu wawili mpaka sasa. (PICHA: eNCA).


Watu wawili wamepoteza maisha na wengine takribani 50 wakifukiwa kwenye vifusi baada ya paa la jengo la maduka lililokuwa linajengwa kuporomoka eneo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban nchini Afrika Kusini.

Watu 29 wameweza kuokolewa kutoka katika jengo hilo.

Madaktari kutoka kampuni ya Netcare 911 walifika kutoa huduma ya kwanza katika eneo hilo la Tongaat.

“Shughuli hii itachukua muda mrefu. Itatuchukua muda kuwafikia wale waliokwama,” alisema msemaji wa kampuni hiyo.

Hata hivyo ni mapema mno kujua sababu ya kuporomoka kwa jengo hilo.

Chanzo: BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad