Tanzania yakamata Shehena kubwa ya Meno ya Tembo kwenye kontena la futi 40 katika bandari ya Zanzibar. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 14, 2013

Tanzania yakamata Shehena kubwa ya Meno ya Tembo kwenye kontena la futi 40 katika bandari ya Zanzibar.

Baadhi ya Pembe za Tembo zilizokamatwa katika bandari ya Malindi  mjini Zanzibar jana (Novemba 13,2013) zikisubiri kuhesabiwa ili kupata idadi kamali na thamani yake na uzito kwa ujumla.

Zoezi likiendelea kupekuwa makunia ya Makombe ya Pwani kutowa magunia yaliohifadhiwa Pembe za Tembo.

Askari wa jeshi la Polisi wakitowa Pembe za Tembo katika makunia wakati wa zoezi hilo jana(Novemba 13,2013) asubuhi katika bandari ya Malindi Zanzibar.
Shehena kubwa ya pembe za tembo ikiwa na vipande 1,021 na uzito wa kilo 2,915  ambayo haijawahi kukamatwa nchini imenaswa  katika bandari ya Zanzibar huku ikishuhudiwa na Mawaziri wa serikali zote mbili wakiongozwa na Waziri wa mali asili na utalii Balozi Khamis Kagasheki.

Shehena hiyo iliyokuwa tayari kusafirishwa kuelekea Philiphine ilikuwa katika magunia 98 yaliyochanganywa na magunia mengine ambayo yalikuwa yamefungwa pamoja na baadhi ya vitu vya baharini, yalikuwa tayari yameshawekwa ndani ya kontena la futi 40 tayari kwa kusafirishwa kwenda Philiphne yakiwa katika hatua za mwisho za mamlaka husika za bandarini.

Wakiongea na wandishi wa habari katika bandari ya Zanzibar ,Waziri wa nchi afisi ya rais utawala bora na idara maalum Bw. Haji Omar Kheri amesema hili ni janga kubwa la nchi na serikali kamwe haitokubali  kuona wahusika wanaanchiwa na kuahidi sheria kufanya kazi yake ,huku kwa upande wake Waziri Kagasheki ambaye aliwisili Zanzibar asubuhii ya Jana(Novemba 13,2013) kushuhudia shehena hiyo amesema ni lazima mtandao utokomezwe kwani utamaliza tembo wa nchii hii na kuipoteza rasilimali ya nchi.

Waziri Kagasheki amesema kuwa kontena hilo lilikuwa likitokea Bandari ya Dar es Salaam na kwamba hadi sasa haijulikani mzigo huo una thamani kiasi gani na kwamba unasadikiwa kumilikiwa na raia wa China.

Tukio hilo linakuja zikiwa ni wiki mbili tangu waziri huyo kukamata pembe za ndovu 706 jijini Dar es Salaam zikimilikiwa na raia wa China.

Pembe hizo 706 ni sawa na tembo 353 waliouawa katika hifadhi za wanyamapori hapa nchini.

Wachina hao walikamatwa katika Mtaa wa Kifaru, Mikocheni wilayani Kinondoni chini ya operesheni iliyoongozwa na Waziri Kagasheki, ambaye aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw.Tarish Maimuna.

Waliokamatwa na shehena hiyo ya pembe za ndovu ni raia watatu wa China, ambao ni Xu Fujie,Chen Jinzha na Huang Qin wote kutoka mji wa Guandung, ambao wamefikishwa mahakamani wiki iliyopita.


Kwa upande wake kamishna wa jeshi la polisi Zanzibar CP Mussa Ali Mussa  amesema polisi imekamata watu wawili wazalendo na inaendelea kuwahoji na kufanya upekuzi nje ya bandari pamoja na kwamba  taarifa zinaonyesha kuwa mzigo huo ni wa raia wa China.

Kamanda wa Kikosi cha Polisi Bandarini Zanzibar akiongoza Operesheni wa kukagua magunia yaliokuwa na Pembe za Tembo yaliokamatwa katika bandari hiyoleo yakiwa katika harakati ya kusafirishwa nje ya Nchi kupitia bandari hiyo, zoezi hilo limefanywa chini ya Jeshi la Polisi Bandari Kikosi cha KMKM, yalikuwa katika Kontena la futi 40.

Operesheni ikiendelea kuhesabu Pembe za Tembo zilizokamatwa katika bandari ya Zanzibar wakiweka hesabu sawa kuhakikisha hesabu iliokamilika na kupata thamani yake halisi.

Magunia haya yakiwa na sehena na makombe ya pwani wakati katikati yakiwa na viroba vya mPembe za Tembo ambayo yakiwa yamehifadhiwa katika Kontena likiwa tayari kusafirishwa nje ya Nchi, limegunduliwa katika bandari ya Zanzibar jana (Novemba 13,2013) asubuhi. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad