Mwili wa Dr.Mvungi kuwasili Nchini Ijumaa Novemba 15 na Kuzikwa Jumatatu Novemba 18 mkoani Kilimanjaro. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 14, 2013

Mwili wa Dr.Mvungi kuwasili Nchini Ijumaa Novemba 15 na Kuzikwa Jumatatu Novemba 18 mkoani Kilimanjaro.

Rais Jakaya Kikwete amewaongoza viongozi na Watanzania katika kutoa mkono wa pole kwafamilia ya marehemu  Daktari Edmund Sengondo Mvungi aliyekuwa mjumbe wa tume ya katiba ambae alifariki dunia nchini Afrika kusini alikokuwa akipata matibabu baada ya kuvamiwa na majambazi na kukatwa mapanga nyumbani kwake Kibamba nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba akitia saini kitabu cha maombelezo ya kifo cha Mjumbe wa Tume hiyo Dkt. Sengondo Mvungi nyumbani kwake Kibamba jijini Dar es Salaam Jana
(Novemba 13,2013).
Tume ya Mabadiliko ya Katiba inawafahamisha wananchi kuwa taratibu za kuusafirisha mwili wa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyefariki nchini Afrika Kusini zimekamilika na mwili wake unatarajia kuwasili nchini siku ya Ijumaa, Novemba 15, 2013.

Baada ya kuwasili, mwili huo utahifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo iliyopo jijini Dar es Salaam.

Aidha, siku ya Jumamosi, Novemba 16, 2013 kutafanyika Ibada ya mazishi katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:00 asubuhi. 

Baada ya misa, marehemu ataagwa katika Viwanja vya Karimjee kuanzia saa 6:30 mchana siku hiyo hiyo ya Jumamosi, Novemba 16, 2013.

Aidha, Marehemu Dkt. Mvungi anatarajiwa kusafirishwa siku ya Jumapili, Novemba 17, 2013 kwenda Kisangara Juu, Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu, Novemba 18, 2013.

Dkt. Mvungi alifariki jana (Jumanne, Novemba 12, 2013) katika Hospitali ya Millpark jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini alikopelekwa kwa ajili ya uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.

Wakati huohuo, Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Joseph Warioba leo (Jumatano, Novemba 13, 2013) wameungana na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kufika nyumbani kwa marehemu Dkt. Mvungi eneo la Kibamba jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa pole kwa familia, ndugu na jamaa wa marehemu Dkt. Mvungi.

Akiwa nyumbani kwa marehemu, rais Kikwete alipata fursa ya kutoa pole kwa familia ya marehemu dokta Mvungi na kisha kusaini kitabu cha kumbukumbu na kutoa pole kwa wafanyakazi wa tume ya katiba akiwemo mwenyekiti wa tume ya katiba jaji mstaafu Joseph Warioba, waziri mkuu mstaafu Daktari Salim Ahamed Salim,jaji mstaafu Agustino Ramadhani na viongozi wengine wa serikali na vyama vya siasa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad