Nchi ya Cameroun yawa Nchi ya 3 toka Afrika kufuzu kwenda Brazil Mwakani kucheza Fainali za Kombe la Dunia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, November 17, 2013

Nchi ya Cameroun yawa Nchi ya 3 toka Afrika kufuzu kwenda Brazil Mwakani kucheza Fainali za Kombe la Dunia.

Hii ni mara ya 6 kwa Cameroun kucheza Fainali za Kombe la Dunia na mara nyingine zikiwa Miaka ya 1982, 1990, 1994, 1998, 2002 na 2010 ambayo ni Rekodi kwa Bara la Afrika.
Nchi ya CAMEROUN leo (Novemba 17,2013) huko Yaounde wameibonda Tunisia Bao 4-1 na kuwa Nchi ya 3 toka Afrika,kufuatia Jana (Novemba 16,2013) ,Nchi ya Nigeria na Ivory Coast  kufuzu kwenda Brazil Mwakani kucheza Fainali za Kombe la Dunia.

Katika mchezo huo Magoli ya Cameroun yamefungwa na Pierre Webo Dakika ya 4,Benjamin Moukandjo  Dakika ya 30,Jean Makoun katika dakika ya  66 & 86 huku goli la Tunisia  likifungwa na Ahmed Akaichi  dakika ya 51.

Hii ni mara ya 6 kwa Cameroun kucheza Fainali za Kombe la Dunia na mara nyingine zikiwa Miaka ya 1982, 1990, 1994, 1998, 2002 na 2010 ambayo ni Rekodi kwa Afrika.

Katika Mechi ya kwanza huko Tunis, Cameroun na Tunisia zilitoka Sare 0-0 lakini leo Cameroun walistahili kwa kila kitu ushindi wao kwa jinsi walivyotawala na kudhibiti Mechi hii huku Nahodha wao Samuel Eto’o leo akiwa mlishaji na mwongozaji mkuu.

Sasa Afrika imeshapata Timu 3 za kwenda Brazil na mbili za mwisho zitapatikana Jumanne kwenye Mechi mbili za mwisho kati ya Algeria na Burkina Faso na Egypt na Ghana.

Senegal 1 Ivory Coast 1 .
AFRIKA  RATIBA/MATOKEO:
Marudiano:-Jumamosi Novemba 16,2013.

Nigeria 2 Ethiopia 0 [Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili 4-1]
Senegal 1 Ivory Coast 1 [Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili 2-4]
Jumapili Novemba 17,2013.
Cameroon 4 Tunisia 1 [Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili 4-1]

[Saa za Bongo]
[Katika Mabano Matokeo Mechi za Kwanza]
Jumanne Novemba 19,2013.

19:00 Egypt v Ghana [1-6]
21:15 Algeria v Burkina Faso [2-3]

**FAHAMU: Washindi 5 ndio watacheza Fainali za Kombe la Dunia

TIMU AMBAZO ZIMEFUZU KWENDA BRAZIL 2014.

[Jumla 24 Bado 8]:

Afika [Nchi 3 Bado 2]: Nigeria, Ivory Coast, Cameroun.

Europe [Nchi 9 Bado 4]: Belgium, Bosnia-Herzegovina, England, Germany, Italy, Netherlands, Russia, Spain, Switzerland.

Nigeria 2 Ethiopia 0 .
South America [Nchi 5, Uruguay wapo kwenye Nchujo]: Argentina, Brazil (Wenyeji), Chile, Colombia, Ecuador.

Asia [Nchi 4, Jordan wapo kwenye Mchujo]: Australia, Iran, Japan, South Korea.

North & Central America/Caribbean [Nchi 3, Mexico wapo kwenye Mchujo]: Costa Rica, Honduras, USA.

**FAHAMU:


- DROO YA KUPANGA MAKUNDI:

-KUFANYIKA TAREHE 6 DESEMBA 2013 Costa do Sauípe Resort, Mata de São João, Bahia, Brazil.

-Kwenye Droo hiyo Timu 7, pamoja na BRAZIL, ambazo ziko juu kwenye Listi ya FIFA ya Ubora Duniani zitawekwa Chungu Na 1 na Timu nyingine 24 zilizobakia zitagawanywa nane nane na kuingizwa Vyungu vingine vitatu na kutenganishwa kutoka Mabara zinakotoka.


-FAINALI KUCHEZWA: 12 Juni 2014 hadi 13 Julai 2014

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad