Habari za Kusikitisha: Dk. Sengondo Mvungi amefariki Dunia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, November 12, 2013

Habari za Kusikitisha: Dk. Sengondo Mvungi amefariki Dunia.

Marehemu Dk. Sengondo Mvungi alipokuwa ICU katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Habari za kusikitisha zilizotufikia jioni hii(Novemba 12,2013) zinasema kuwa Dk. Sengondo Mvungi amefariki dunia katika Hospitali ya Milpark Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa. 

Dk. Mvungi alipelekwa wiki iliyopita Nov. 7 mwaka huu kwa ajili ya kupewa matibabu zaidi akitokea Hospitali ya Muhimbili kitengo cha MOI ambako muda wote alikuwa hajitambui baada ya kushambuliwa na majambazi na kuumizwa vibaya sehemu ya kichwani akiwa nyumbani kwake Kibamba. 

Dakta Sengodo Mvungi
enzi za uhai wake.
Wakati Dk. Mvungi anafariki, jana (Novemba 11,2013) Jeshi la Polisi, kupitia  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi, lilitangaza kuwakamata watuhumiwa 9 wakiwa na mapanga yaliyotumika katika uvamizi huo.

Mpaka mauti yanamfika, Dk. Mvungi alikuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini na Mhadhiri Mwandamzi wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Bagamayo (UB).

Marehemu aliwahi kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI - AMEEN!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad