Timu ya soka ya Taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes imeanza vizuri michuano ya Kombe la Chalenji baada ya kuichapa Sudan Kusini kwa mabao 2-1. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, November 27, 2013

Timu ya soka ya Taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes imeanza vizuri michuano ya Kombe la Chalenji baada ya kuichapa Sudan Kusini kwa mabao 2-1.

Zanzibar Heroes imeshinda mechi yake hiyo ya ufunguzi dhidi ya Sudan Kusini kwenye Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi, leo… Chalenji ya msimu huu 2013/2014 inatazamiwa kuwa na mvuto wa aina yake kutokana na vikosi vilivyosukwa ingawa sekretarieti ya Cecafa imeonyesha wasiwasi kutokana na mashabiki wa hapa kutokuwa na tabia ya kuhudhuria viwanjani.
Timu ya soka ya Taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes leo(Novemba 27,2013)  imeanza vizuri michuano ya Kombe la Chalenji  baada ya kuichapa Sudan Kusini kwa mabao    2-1.

Zanzibar Heroes imeshinda mechi yake hiyo ya ufunguzi dhidi ya Sudan Kusini kwenye Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi, leo.

Mechi hiyo ilikuwa nzuri na  Zanzibar wakitawala zaidi na kama wangekuwa makini basi wangeweza kushinda mabao mengi zaidi.

Zanzibar  ndio walitangulia kufunga mabao yote mawili kabla ya Sudan Kusini kupata la kufutia machozi.

Nao wenyeji wa Mashindano hayo, Kenya, Harambee Stars wameanza vibaya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Ethiopia katika mchezo wa Kundi A, Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.

Matokeo hayo yanaifanya Zanzibar iliyoshinda 2-1 mchezo wake wa kwanza dhidi ya Sudan Kusini iongoze Kundi na kujiweka katika mazingira mazuri ya kuingia Robo Fainali.

Ethiopia waliitesa Kenya kwa soka ya ‘Kibarcelona’, huku wachezaji wa Harambee wakitumia nguvu zaidi na maarifa haba.

Allan Wanga alijaribu sana kuisumbua ngome ya Ethiopia, lakini bahati haikuwa yake jioni ya leo.

Kocha wa Kenya, Adel Amrouche Mbelgiji mwenye asili ya Algeria, hakuwepo kwenye benchi leo kuiongoza timu yake na habari zinasema amekerwa na kitendo cha wachezaji wake kutopewa posho kwa muda wote wa kuwa kambini kujiandaa na mashindano.

Chalenji ya msimu huu inatazamiwa kuwa na mvuto wa aina yake kutokana na vikosi vilivyosukwa ingawa sekretarieti ya Cecafa imeonyesha wasiwasi kutokana na mashabiki wa hapa kutokuwa na tabia ya kuhudhuria viwanjani.

Kesho (Novemba 28,2013) Kilimanjaro Stars iliyoko Kundi B, itacheza mechi yake ya kwanza Alhamisi kwa kuikabili Zambia jioni kwenye Uwanja wa Kenyatta mjini Machakos.

Mbali na mechi ya Stars mchezo mwingine wa kundi hilo utakuwa baina ya Burundi na Somalia mjini humo.

Stars, Uganda, Kenya na Ethiopia ndiyo timu zinazozungumzwa zaidi mjini Nairobi kutokana na uimara wake.


Pia mchezo wa kesho baina ya Kilimanjaro Stars na Zambia unatarajiwa kuwa na upinzani mkali kutokana na historia ya timu hizo mbili katika michuano hiyo.

MAKUNDI:
Kundi A
KUNDI B
KUNDI C
-Kenya
-Ethiopia
-Zanzibar
-South Sudan

-Tanzania Bara
-Zambia
-Burundi
-Somalia
-Uganda
-Rwanda
-Sudan
-Eritrea
**FAHAMU: Timu mbili za Juu kila Kundi zitasonga Robo Fainali pamoja na Washindi wa Tatu wawili Bora.
RATIBA:
TAREHE
NA
MECHI
KUNDI
UWANJA
SAA
Jumatano Novemba 27
1
Zanzibar v South Sudan
A
Nyayo
1400
2
Kenya v Ethiopia
A
Nyayo
1630
Alhamisi Novemba 28
3
Burundi v Somalia
B
Machakos
1400
4
Tanzania Bara v Zambia
B
Machakos
1600
Ijumaa Novemba 29
5
Sudan v Eritrea
C
Machakos
1400
6
Uganda v Rwanda
C
Machakos
1600
Jumamosi Novemba 30
7
Ethiopia v Zanzibar
A
Nyayo
1400
8
South Sudan v Kenya
A
Nyayo
1600
Jumapili Desemba 1
9
Somalia v Tanzania
B
Nyayo
1400
10
Zambia v Burundi
B
Nyayo
1600
Jumatatu Desemba 2
11
Sudan v Rwanda
C
Machakos
1400
12
Eritrea v Uganda
C
Machakos
1600
Jumanne Desemba 3
13
South Sudan v Ethiopia
A
Machakos
1400
14
Kenya v Zanzibar
A
Machakos
1600
Jumatano Desemba 4
15
Tanzania v Burundi
B
Nyayo
1400
16
Somalia v Zambia
B
Nyayo
1600
Alhamisi Desemba 5
17
Rwanda v Eritrea
C
Nyayo
1400
18
Uganda v Sudan
C
Nyayo
1600
Ijumaa Desemba 6
MAPUMZIKO
ROBO FAINALI
Jumamosi Desemba 7
19
C1 v B2
Mombasa
BADO
20
A1 v 3 BORA 1
Mombasa
BADO
Jumapili Desemba 8
21
B1 v 3 BORA 2
Mombasa
BADO
22
A2 v C2
Mombasa
BADO
Jumatatu Desemba 9
MAPUMZIKO
Jumanne Desemba 10
NUSU FAINALI
23
Mshindi 19 v Mshindi 20
BADO
24
Mshindi 21 v Mshindi 22
BADO
Desemba 11
MAPUMZIKO
Alhamisi Desemba 12
25
Mshindi wa Tatu
1400
26
FAINALI
1600

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad