Kipa Juma Kaseja achwa kwenye Kikosi cha Kilimanjaro Stars kinachoenda kushiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayofanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27 mwaka huu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 21, 2013

Kipa Juma Kaseja achwa kwenye Kikosi cha Kilimanjaro Stars kinachoenda kushiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayofanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27 mwaka huu.


Kocha Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 23 watakaoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayofanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27 mwaka huu…huku  imepangwa kundi B katika michuano ya mwaka huu itacheza mechi yake ya kwanza Novemba 28 mwaka dhidi ya Zambia kwenye Uwanja wa Machakos.


Michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika  Mashariki na Kati (Cecafa) ya  Chalenji, inaanza kutimua vumbi wiki ijayo ikishirikisha timu 12.

Michuano hiyo inafanyika nchini Nairobi nchini Kenya huku Tanzania yenye timu mbili ikiwa miongoni mwa washiriki.

Katika kuhakikisha michuano hiyo inakuwa na msisimko huku waandaaji wameialika Taifa ya Zambia kwenye michuano hiyo.

Tanzania itawakilishwa na Taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars  na Zanzibar (Zanzibar Heroes), timu hizo tayari zipo kambini zikiajiandaa kwa ajili ya michuano hiyo.

Kilimanjaro Stars, ipo kundi B imepangwa katika kundi moja na timu za Burundi, Zambia na Somalia.

Zanzibar iko kundi (A)pamoja na wenyeji Kenya, Ethiopia, Sudani Kusini.

Aidha Kocha Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 23 watakaoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayofanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27 mwaka huu.

Kilimanjaro Stars iliyotwaa kombe hilo mara ya mwisho mwaka 2010 chini ya Kocha Jan Poulsen, na ambayo imepangwa kundi B katika michuano ya mwaka huu itacheza mechi yake ya kwanza Novemba 28 mwaka dhidi ya Zambia kwenye Uwanja wa Machakos.

Wachezaji wanaounda kikosi hicho cha Tanzania Bara ni makipa Deogratius Munishi (Yanga), Ivo Mapunda (Gor Mahia, Kenya) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Michael Pius (Ruvu Shooting) na Said Moradi (Azam).

Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Ramadhan Singano (Simba) na Salum Abubakar (Azam).

Safu ya ushambuliaji inaundwa na Elias Maguli (Ruvu Shooting), Faridi Musa (Azam), Joseph Kimwaga (Azam), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngasa (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).

Kilimanjaro Stars inatarajia kuondoka Jumatatu (Novemba 25 mwaka huu) kwenda Nairobi kushiriki michuano hiyo itakayoanza Novemba 27 mwaka huu na kumalizika Desemba 13 mwaka huu.   

Kikubwa kwetu Watanzania ni kuziombea dua timu hizo mbili ziweze kufanya vizuri, ikiwezekana  kupata ushindi wa kwanza na wa pili. 

Bingwa Mtetezi wa Chalenji Cup ni Uganda ambao walitwaa Kombe Mwaka Jana lilipochezwa Nchini kwao kwa kuifunga Kenya Bao 2-1 katika Fainali.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad