Cristiano Ronaldo apiga Hetitriki yake ya 23 kwa Real Madrid wakati Klabu yake hiyoilipoitwanga Real Sociedad Bao 5-1 kwenye Mechi ya La Liga. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, November 09, 2013

Cristiano Ronaldo apiga Hetitriki yake ya 23 kwa Real Madrid wakati Klabu yake hiyoilipoitwanga Real Sociedad Bao 5-1 kwenye Mechi ya La Liga.



Ronaldo: I do my talking on the pitch.
Cristiano Ronaldo leo(Novemba 09,2013) amepata Hetitriki yake ya 23 kwa Real Madrid wakati Klabu yake hiyoilipoitwanga Real Sociedad Bao 5-1 kwenye Mechi ya La Liga.

Ronaldo ndie aliefunga Bao la kwanza kabla kumlisha Karim Benzema kufunga Bao la Pili na kufuatia Penati aliyofunga Ronaldo Bao la 3 kwa Real.

MAGOLI.

Real Madrid 5 

-Ronaldo Dakika ya 12, 26 (Penati), & 76

-Benzema 18

-Khedira 36

Real Sociedad 1 

-Griezmann 61

Gareth Bale akamtengenezea Sami Khedira kupiga Bao la 4 na Real Sociedad wakapata Bao lao moja Mfungaji akiwa Antoine Griezmann.

Ronaldo alifunga Bao lake la 3 kwenye Mechi hii na la 5 kwa Real kwa frikiki safi.

Ushindi huu umewafanya Real, walio Nafasi ya 3 na wakiwa wamecheza Mechi moja zaidi, kufikisha Pointi 31 na mbele yao wapo Atletico Madrid wenye Pointi 33 na Barcelona Pointi 34.

LA LIGA:-RATIBA/MATOKEO:

[Saa za Bongo]

Ijumaa Novemba 8

Granada CF 3 Malaga CF 1

Osasuna 0 Almeria 1

Jumamosi Novemba 9

Real Madrid 5 CF Real Sociedad 1

2000 Getafe v Elche

2200 Athletic de Bilbao v Levante

0000 Celta de Vigo v Rayo Vallecano

Jumapili Novemba 10

1400 RCD Espanyol v Sevilla FC

1900 Valencia v Real Valladolid

2100 Villarreal v Atletico de Madrid

2300 Real Betis v FC Barcelona

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad