Chelsea itabidi wamshukuru Refa Andre Marriner kwa kuwaokoa toka kwenye kipigo kwa Penati tata katika Dakika ya 93 wakati West Brom wanaongoza Bao 2-1. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, November 09, 2013

Chelsea itabidi wamshukuru Refa Andre Marriner kwa kuwaokoa toka kwenye kipigo kwa Penati tata katika Dakika ya 93 wakati West Brom wanaongoza Bao 2-1.



Chelsea drew 2-2 at home with West Brom on Saturday after a 96th-minute Eden Hazard penalty saved a Premier League point for Jose Mourinho's men at Stamford Bridge.

Leo (Novemba 09,2013) wakiwa nyumbani katika uwanja wao Stamford Bridge, Chelsea itabidi wamshukuru Refa Andre Marriner kwa kuwaokoa toka kwenye kipigo baada ya kuwapa Penati tata katika Dakika ya 93 wakati West Brom wanaongoza Bao 2-1.

Penati hiyo ilitolewa na Refa huyo baada ya Mchezaji wa Chelsea Ramires kuanguka baada kugongana na Steven Reid na Penati hiyo kufungwa na Eden Hazard.

Chelsea ndio walitangulia kufunga katika Dakika ya 45 kwa Bao la Samuel Eto'o lakini Kipindi cha Pili West Brom wakafunga Bao mbili kupitia Shane Long Dakika ya 60 na Stephane Sessegnon Dakika ya 68.

Baada Dakika 90 kwisha Bango likaonyesha Dakika 4 za nyongeza na ndipo Dakika ya 93 ikaja Penati tata iliyolinda Rekodi ya Jose Mourinho ya kutofungwa Nyumbani kwenye Ligi.

Liverpool were scintillating going forward and Steven Gerrard's dangerous free-kick went in off Fernando Amorebieta to put them in front, before Martin Skrtel headed home a Gerrard corner to score his first goal since he struck in a 4-0 victory against the same opposition last December.
Nao Wakiwa kwao Anfield, Liverpool wameifumua Fulham Bao 4-0 kwa Bao za Fernando Amorebieta, kwa kujifunga mwenyewe, Martin Skrtel  na Bao mbili za Luis Suárez.

Ushindi huu umeifanya Liverpool wakamate Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 nyuma ya Arsenal.

LIGI KUU ENGLAND:-RATIBA/MATOKEO.
Jumamosi Novemba 9,2013.

Aston Villa 2 Cardiff 0

Chelsea 2 West Brom 2

Crystal Palace 0 Everton 0
 
Liverpool 4 Fulham 0

Southampton 4 Hull City 1

LIGI KUU ENGLAND RATIBA:-Jumapili Novemba 10,2013.

15:00 Tottenham v Newcastle

17:05 Sunderland v Man City

19:10 Man United v Arsenal

19:10 Swansea v Stoke
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad