Bibi Kizee:Navuta sigara 15 kwa Siku. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, November 15, 2013

Bibi Kizee:Navuta sigara 15 kwa Siku.



Bi.Dorothy Howe.

Huko SUSSEX, Nchini Uinngereza,Bibi Kizee mwenye  umri wa miaka 100 ameibuka na kusema kuwa amevuta sigara laki tano tangu akiwa msichana mdogo.

Dorothy Howe ambaye ni katibu muhtasi mstaafu kutoka Uingereza alisema alianza kuvuta sigara tangu akiwa na umri wa miaka 16 na tabia hiyo ameendelea nayo hadi leo.

Alisema kwa kuvuta kwake sigara ametumia pauni 193,000 (zaidi ya sh. milioni 400) ambapo pia hutumia pombe kali aina ya whisky katika maisha yake.

Alipoulizwa kama ana mpango wa kuacha kuvuta sigara ajuza huyo alisema kuwa hataacha bali ataendelea na starehe yake hiyo hadi zipande bei.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad