Utafiti mpya unasema bado kuna Watu milioni 774 Duniani wasiojua Kusoma na Kuandika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, September 28, 2013

Utafiti mpya unasema bado kuna Watu milioni 774 Duniani wasiojua Kusoma na Kuandika.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi wa Tanzania Mhe.Shukuru Kawambwa akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Mikakati walioiweka pamoja na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar juu ya kushirikiana na Tume ilioundwa ya kuchunguza matokeo ya Mitihani ya wanafunzi wa Kidato cha Nne,hafla iliofanyika katika Ukumbi wa  Wizara ya Elimu Zanzibar.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Elimu, Sayansi na Utamaduni Unesco, lilitoa ripoti wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kujua Kusoma na Kuandika Septemba 8 mwaka huu, iliyosema idadi kubwa ya watu hao mbumbumbu wanaishi katika mabara ya Afrika na Asia.

Pia takwimu za ripoti zinaonyesha kuwa robo tatu ya wale wasiojua kusoma na kuandika ni wanawake, na kwamba hali hiyo inaweza kuongezeka hata wakati wa kufikiwa tarehe ya mwisho ya malengo ya Maendeleo ya Milenia ambayo ni mwaka 2015.

Katika ujumbe wake kuadhimisha siku hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Irina Bokova  alisema kuwa dunia inapaswa kujikagua upya.

Alisema kuwa dunia ina wajibu wa  kuboresha mifumo yake ya utoaji wa elimu, kwani bila kufanya hivyo kuna uwezekano wa kurudi  nyuma kimaendeleo. “ Tunapaswa kumulika mifumo yetu ya utoaji elimu ili iende sambamba na mahitaji ya wakati” anasema.

Wasiojua kusoma na kuandika Tanzania.

Ripoti hiyo ya Unesco imetolewa katika wakati ambapo kiwango cha kujua kusoma na kuandika nchini kikitajwa kuporomoka.Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2002 idadi ya Watanzania wasiojua kusoma na kundika ilifikia milioni 6.2.

Akizungumza bungeni, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa alisema kuwa  idadi hiyo ni kwa watu wenye umri wa miaka 15 na kuendelea, sawa na asilimia 31.

Aliongeza kusema kuwa  kuna uwezekanano idadi hiyo ikaongezeka kutokana na mazingira yaliyopo sasa.

Alieleza kuwa watu wasiojua kusoma na kuandika hawajamalizika, na kwamba Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012  bado haikuwa imetoa  mchanganuo wa watu wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Ili kuimarisha Elimu ya Watu Wazima, Serikali inatekeleza mambo mbalimbali, ikiwemo kuboresha mpango wa awali wa Elimu ya Watu Wazima kupitia programu ya ‘Ndiyo Naweza’ yenye lengo la kupunguza idadi ya wasiojua kusoma na kuandika nchini’’ anasema na kuongeza:-

Serikali inatumia uzoefu uliopatikana katika utekelezaji wa Mpango wa Uwiano Kati ya Elimu ya Watu Wazima na Jamii (MUKEJA), ambapo mpaka mwaka 2012 ulikuwa na jumla ya wa 

Wahitimu darasa la saba.

Pamoja na kuwepo kwa mikakati anayotaja Waziri Kawambwa, hali katika ngazi ya elimu ya msingi haijawa nzuri.  

Tafiti zinaonyesha kuna idadi kubwa ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi bila ya kujua kusoma na kuandika. 

Cha kushangaza baadhi ya wanafunzi hao wamekuwa wakichaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari.

Kwa mfano, Aprili mwaka jana, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ilibaini kuwepo kwa wanafunzi wa sekondari 5200 waliokuwa hawajui kusoma na kuandika.

Wanafunzi hao walikuwa sehemu ya wahitimu wa darasa la saba mwaka 2011.

Awali mwaka 2010, asasi isiyo ya kiraia ya Twaweza ilitoa ripoti ya utafiti iliyobainisha kuwa kati ya wahitimu watano wa darasa la saba, mmoja hawezi kusoma hadithi ya kiwango cha darasa la pili.

Utafiti huo uliopewa jina la ‘Are Our Children Learning’ (Je, watoto wetu wanajifunza), ulishirikisha sampuli ya watoto 42,033 kutoka kaya 22,800 nchi nzima.

Mikakati ya Nchi.

 Tanzania imekuwa ikitekeleza mipango mbalimbali yenye shabaha ya kuinua kiwango cha watu kujua kusoma na kuandika. 

Miongoni mwa mipango hiyo ni ule ulianzishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1961ambao unatajwa kuwa ndiyo ulioweka misingi ya hali ya elimu nchini. 

Idadi kubwa ya watu ilijitokeza na kujiunga katika taasisi za mafunzo ya watu wazima.

Mpango mwingine ulitekelezwa katika kipindi cha mwaka 1964 hadi 1969, na kuweka  mkazo wa kuboresha na kuinua elimu ya watu wazima, au maarufu ‘ngumbaru’ enzi hizo.

Kupitia mipango hiyo ya uendelezaji wa elimu wa watu wazima, inaelezwa kwamba hadi kufikia miaka ya 1980, Tanzania ilikuwa ni moja ya nchi kadhaa duniani ambazo watu wake wengi walikuwa wanajua kusoma na kuandika.

Kutokana na hali hiyo, Umoja wa Mataifa uliitaja Tanzania kuwa ni moja ya nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara ambayo imefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuteleleza mikakati ya kupunguza hali ya kutojua kusoma na kuandika.

Sio kutajwa tu, Tanzania pia ilipewa tuzo maalumu kwa mafanikio hayo, ambayo watu wengi wanayanasibisha na dhamira ya dhati aliyokuwa nayo Rais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Nyerere.

Mafanikio hayo yalichangiwa pia na uanzishwaji wa kampeni iliyoendeshwa katika maeneo ya vijijini ambako ndiko kulikokuwa na idadi kubwa ya watu wasiojua kusoma na kuandika .

Nakisomo 907,771.’ Cha kushangaza inaelezwa kwamba kiwango cha kujua kusoma na kuandika nchini, sasa kimeshuka kutoka asilimia 89.4  mwaka 1986 hadi kufikia asilimia 69  mwaka 2010.

Baadhi ya wataalamu wa elimu wanasema kuwa idadi hiyo inaweza kuongezeka  zaidi katika kipindi cha miaka mitano ijayo kutokana na mwelekeo mpya wa sekta ya elimu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad