Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu kwenda jela jumla ya miaka 13, washtakiwa
watatu katika kesi ya wizi wa Sh1.1 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje
(EPA).
Akitoa
hukumu hiyo jana kwa niaba ya wenzake, Jaji Sekela Mushi na Sam
Rumanyika,Msajili Lameck Mlacha alisema mshtakiwa Bahati Mahenge atatumikia
kifungo cha miaka saba jela.
Mshtakiwa
Manase Makale atatumikia kifungo cha miaka mitano jela na mkewe ambaye ni
mshtakiwa katika kesi hiyo, Edda Makale atatumikia kifungo cha mwaka mmoja na
nusu.
Washtakiwa
wawili kwenye kesi hiyo iliyosikilizwa kwa miaka mitano, Davis Kamungu na
Godfrey Mushi waliachiwa huru baada ya mahakama kuwaona hawana hatia.
Mbali na
kutoa hukumu hiyo, aliamuru mshtakiwa Bahati Mahenge na Manase Makale kurejesha
kiasi cha Sh1,186,534,303.27 walichodaiwa kukiiba katika akaunti EPA,iliyopo
Benki Kuu ya Tanzania (BOT).
Akiendelea
kusoma hukumu hiyo, Mlacha aliwaachia huru washtakiwa Davis Kamungu na Godfrey
Mushi baada ya kuwaona hawana hatia kutokana na upande wa mashtaka kushindwa
kuthibitisha pasipo kuacha shaka mashtaka dhidi yao.
Kabla ya hukumu hiyo
kutolewa, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Shadrack Kimaro aliiambia mahakama
kuwa upande wa mashtaka hauna rekodi za uhalifu za washtakiwa hao.
Kimaro
aliiomba mahakama kutumia mamlaka yake chini ya kifungu cha 348(1) na cha
358(1) cha mwenendo wa mashauri ya jinai sura ya 20 kuwaamuru washtakiwa
waliotiwa hatiani kurejesha fedha walizochukua na kuisababishia Serikali
hasara.






No comments:
Post a Comment