Usiache kufanya biashara na zitafute fadhila za Mwenyezi Mungu kwa Kujituma na kufanya kazi ni moja ya sababu muhimu za ustawi wa kiuchumi na kijamii wa jamii. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 17, 2013

Usiache kufanya biashara na zitafute fadhila za Mwenyezi Mungu kwa Kujituma na kufanya kazi ni moja ya sababu muhimu za ustawi wa kiuchumi na kijamii wa jamii.

Kazi ni haki ya msingi na ni jambo zuri kwa mwanadamu katika kuyamudu na kuyaendeleza maisha yake yaweze kuendana na mpango mzima wa kuumbwa kwake. Kazi kimsingi inamsaidia na kumpa mtu thamani ya utu, na jinsi anavyopaswa kufanya ili utu wake uendelee kuthaminiwa. 
Miongoni mwa mambo yanayokwamisha ustawi na maendeleo ya jamii ni uvivu, utumiaji wa madawa ya kulevya na uhalifu.
   
Hii leo nafasi ya mtaji wa mwanadamu au nguvu kazi katika kukua na kupatikana maendeleo ya kiuchumi ni miongoni mwa mambo muhimu na ya kimsingi mno katika uchumi mkubwa. 
Kimsingi kujituma na kufanya kazi ni uga wa nguvu na uwezo . Kadiri taifa fulani litakavyojituma katika uga wa hima na kufanya kazi ndivyo mazingira ya kufikia ustawi na maendeleo yatakavyoandaliwa zaidi.

Kwa kweli wale ambao hawana ajira ama ajira yao ni ya kiwango cha chini wanapata mateso yanayoletwa na hali hiyo katika utu na wengine wote wanaokutana na magumu makubwa kila wanapojaribu kutafuta nafasi yao katika ulimwengu wa ajira kama hawa Wafanya biashara wa Ndizi wilayani Ngara mkoani Kagera.
Msingi wa maisha umesimama juu ya hima na kufanya kazi na uzima wa kiroho na kimwili wa mtu na jamii nao unapatikana kwa kuwa na maisha na uchumi salama.

Kwa msingi huo katika mkusanyiko salama, wanajamii wote kila mmoja anapaswa kuwa na hisa yake katika uga wa uzalishaji bidhaa na utoaji huduma na kuwa na nafasi muhimu katika ushiriki wa masuala ya kijamii.

Kadiri roho na moyo wa hima na kufanya kazi utakavyokuwa imara na madhubuti katika jamii, ndivyo ambavyo uwanja wa kuongezeka uzalishaji huandaliwa na matokeo yake kuwa ni kukua zaidi uchumi jambo ambalo bila shaka lina manufaa makubwa kwa jamii yoyote ile.

Katika uga wa mtu binafsi, kuna mlolongo wa mahitaji ya mtu kuanzia chakula na mavazi hadi kupata daraja katika jamii ambapo mambo haya humsukuma mtu kujituma na kuwa na bidii katika kufanya kazi ili aweze kukidhi mahitaji yake ya kimaisha.

Katika uga wa kijamii pia hutokea anga ya ushindani wa wanajamii kwa ajili ya kujipatia kipato, ushirikiano wa wanajamii na hivyo kukuza roho ya kazi hima na bidii katika jamii.

Tunashuhudia leo katika jamii zetu, mtu ambaye hana kazi na ambaye anazurura na kuranda randa tu mitaani, hana hadhi wala heshima kwa majirani na hata katika jamii anayoishi.

Lakini mtu mwenye kazi yake huheshiwa na kuonekana mtu mwenye heshima na hadhi katika jamii.

Utamaduni na mafundisho ya vitabu vya mungu vinatoa wito wa kuweko ushirikiano wa pamoja wa wanajamii na hima za pamoja na yanawataka wanajamii kufanya hima na bidii katika kazi na kutofikiria maslahi yao binafsi bali kutanguliza mbele maslahi ya wote.

Natija ya kuweko mtazamo kama huu huleta roho na moyo wa mfungamano katika jamii.

Ukweli wa mambo ni kuwa, kila mwanaadamu ananufaika na kustafidi na matunda ya mwenziwe na hakuna mtu anayeweza kuishi katika jamii bila ya kumtegemea mwenzake hata kama atakuwa na utajiri wa kutupa; kwani ili aweze kufanyiwa kazi fulani hana budi kumuajiri mtu. 

Hivyo tunaweza kusema kuwa, mtu anapaswa kuwa yuko kwa ajili ya jamii kabla ya kuwa yuko kwa ajili yake.

Licha ya kuwa maendeleo ya kiteknolojia yamekuja na kuchukua kwa kiwango kikubwa kazi za mwanadamu, lakini tunapaswa kusema kuwa, teknolojia yenyewe ni natija ya kazi na ubunifu wa mwanadamu.

Endapo mazingira ya kazi hayatoandaliwa basi watu wenye vipaji hawatoweza kuleta uwanjani uwezo wao na kustafidi na suhula zilizoko kwa ajili ya ustawi na maendeleo.


Hima na kufanya kazi ni dhamana ya kubakia na kuongezeka kwa mali na mtaji. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad