Real Madrid wamepoteza baada ya kuchwapwa kwao Bao 1-0 na Atletico Madrid na kuimaliza ile Rekodi ya kutoifunga Real Madrid kwenye La Liga tangu Mwaka 1999 zikiwa ni Mechi 23. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 29, 2013

Real Madrid wamepoteza baada ya kuchwapwa kwao Bao 1-0 na Atletico Madrid na kuimaliza ile Rekodi ya kutoifunga Real Madrid kwenye La Liga tangu Mwaka 1999 zikiwa ni Mechi 23.

Real Madrid wamepoteza El Derbi Madrileno baada ya kuchwapwa kwao Santiago Bernabeu Bao 1-0 na Atletico Madrid ambao Jana walimaliza ile Rekodi ya kutoifunga Real kwenye La Liga tangu Mwaka 1999 zikiwa ni Mechi 23.
Bao la ushindi kwa Atletico lilifungwa na Mbrazil Diego Costa katika Dakika ya 11.

Ushindi huo umewafanya Atletico wabaki kileleni wakifungana kwa Pointi na FC Barcelona, ambao Jana (sEPTEMBA 28,2013) waliifunga Almeria Bao 2-0, na wote sasa wana Pointi 21 kila mmoja baada Mechi 7 lakini Barca wako juu kwa ubora wa Magoli.

Real wamebaki Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 5 nyuma.

Katika Mechi ya Barcelona na Almeria, Lionel Messi aliifungia Barca Bao la kwanza lakini akalazimika kutoka baada ya kupata matatizo ya Musuli.

Bao la Pili la Barca lilifungwa na Adriano.


Borussia Dortmund continued their fine start to the
season with a comfortable 5-0 home
win over 10-man Freiburg on Saturday.
Huko Germany kwenye Bundesliga, Vinara Borussia Dortmund waliinyuka Freiburg Bao 5-0 na Mabingwa Watetezi Bayern Munich kuifunga VfL Wolfsburg 1-0.

Bao za Dortmund zilifungwa na Marco Reus na Robert Lewandowski, Bao 2 kila mmoja na Jakub Blaszczykowski kupiga Bao la tano.

Kwenye Mechi ya Bayern Munich, Thomas Muller ndie aliefunga Bao pekee.

Matokeo hayo yanaifanya Dortmund ikamate usukani ikiwa na Pointi 19 sawa na Bayern Munich ambao wako Nafasi ya Pili kwa kuzidiwa ubora wa magoli.

RESULTS

Huko Italy kwenye Serie A. AC Milan na Napoli zote zilishinda kwa AC Milan kuipiga 1-0 Sampdoria kwa Bao la Birsa na Napoli kuichapa Genoa 2-0 Bao zote zikifungwa na Pandev.






RESULTS

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad