Ni moto, moto kila mahali....''siri na baadhi ya wanavijiji ambao ni wavivu wa kusafisha mashamba yao kabla ya mvua hazijanyesha’’. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 24, 2013

Ni moto, moto kila mahali....''siri na baadhi ya wanavijiji ambao ni wavivu wa kusafisha mashamba yao kabla ya mvua hazijanyesha’’.

Licha ya Halmashauri za Wilaya za Ngara na Biharamulo Mkoani Kagera  kutoa elimu ya mazingira kwa wanavijiji na hata kuwasaidia kuanzisha kamati za mazingira katika kila kijiji, ‘’utamaduni’’ wa kuchoma misitu wakati wa kiangazi bado haujawatoka wanavijiji hao.

Muonekano wa Vilima kadhaa ndani ya wilaya ya Ngara ,Biharamulo na hata Karagwe mkoani Kagera vimekuwa na vipara kwa sababu ya uchomaji moto huo pamoja na uharibifu wa Mazingira.

Katika Vijiji  vilivyo pembezoni mwa Barabara kuu ya Rwanda,Burundi hadi Isaka:-Camera ya Mwana wa Makonda Blog  ilijionea kilomita kwa kilomita za msitu ulioteketezwa kwa moto na miti kukatwa.

‘’Sababu nyingine ambayo ilitolewa, na ambayo ina uzito kidogo, ni kwamba uchomaji huo unafanywa kwa siri na baadhi ya wanavijiji ambao ni wavivu wa kusafisha mashamba yao kabla ya mvua hazijanyesha’’

Mabadiliko ya tabianchi (climate change), uharibifu wa vyanzo vya maji unaofanywa na wafugaji, na tabia hiyo chafu ya wenyeji ya kuchoma misitu, vinaliangamiza kwa kasi kikubwa Mazingira yetu.

Japo ni wachache; lakini wakiadhibiwa vikali kama mfano kwa wengine, italeta woga kwa wanavijiji wengine kuendelea na utamaduni huo mchafu unaoteketeza misitu yenye miti mingi.
Kumekuwa na makabila makubwa  yanayoishi  pembezoni mwa Barabara hiyo lakini Si rahisi kufahamu ni lipi kati ya hayo ambalo limebobea katika tabia hiyo chafu ya uchomaji misitu.

Katika kutafuta ni kwa nini hasa wenyeji hupendelea kuchoma misitu wakati wa kiangazi, Nlipewa majibu tofauti na yenye utata. Kwa mfano, wanavijiji kadhaa, walidai kwamba baadhi ya wanavijiji huchoma moto misitu ili kuwawinda kirahisi wanyama wanaokimbia moto japo ukweli hakuna wawindaji.

Hoja hii haina uzito wowote, kwa sababu makabila yote yanayopatikana si wawindaji,”shughuli zao kuu ni kilimo na  ufugaji …. Kwa hiyo, hawezi kuwa wanachoma moto misitu  kwa sababu za uwindaji, kwa kuwa kiasili si shughuli yao.”

Katika baadhi ya vijiji vya Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, ilitolewa hoja nyingine kwamba baadhi ya wenyeji huchoma moto misitu wakati wa kiangazi ili mvua zikinyesha wakati wa masika nyasi nzuri ziote na kwa haraka.

Hoja hiyo nayo imekuwa ikitumiwa sana na kwa kisingizio cha kuchoma moto ili nyasi nzuri ziote.

‘’Sababu nyingine ambayo ilitolewa, na ambayo ina uzito kidogo, ni kwamba uchomaji huo unafanywa kwa siri na baadhi ya wanavijiji ambao ni wavivu wa kusafisha mashamba yao kabla ya mvua hazijanyesha’’.

Inaaminika kwamba moto unawashwa kwa siri na wanavijiji hao katika mashamba yao, lakini baadaye husambazwa na upepo na kuingilia misitu inayopakana na mashamba hayo na kuiteketeza.

Hoja hii inaweza kuwa na mantiki kidogo, lakini kama nilivyoeleza mwanzo, tabia hiyo chafu inatokana na uvivu na Uduni wa Elimu ya Mazingira.

Je, Halmashauri za Wilaya Mkoani Kagera na serikali za vijiji, wanafanya nini kupambana na wanavijiji hao wachache wavivu na wajinga wanaoteketeza misitu  kwa moto na Kukata Miti hovyo?

Jibu ni kwamba, japo sheria ndogo ndogo zimetungwa na kupitishwa katika baadhi ya vijiji kukabiliana nao; lakini si rahisi kuwakamata kwa kuwa jambo hilo hufanyika kwa siri mno na msituni.

Moto ukiwaka na nyote mkakimbilia huko, bado si rahisi kufahamu nani aliuanzisha. Na hata kama mtafanya uchunguzi baadaye, itakuwa bado si rahisi kumfahamu mhusika,” anasema ofisa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya NgaraBw.Thoba Mhina,alipokaririwa Kupitia Mjdala wa asubuhi njema wa Radio Kwizera FM.

Chanzo cha kitendo hicho kiovu ni ujinga, na chanzo cha ‘utamaduni’ huo hovyo wa kuchoma moto misitu ni ujinga,  na ndiyo maana elimu zaidi kwa wanavijiji hao ndiyo njia pekee ya kukomesha tabia hiyo.

Lakini pia ni muhimu sheria ndogo ndogo zinazopitishwa na vijiji na kubarikiwa na Halmashauri za wilaya, zikatumika kuwaadhibu wale wachache wanaokamatwa, pasi shaka yoyote, wakichoma moto misitu.

Japo ni wachache; lakini wakiadhibiwa vikali kama mfano kwa wengine, italeta woga kwa wanavijiji wengine kuendelea na utamaduni huo mchafu unaoteketeza misitu yenye miti mingi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad