TASWIRA :- Hali ilivyokuwa baada ya Bomu lililolipuka kwenye mkutano wa Chadema katika eneo la Soweto, huku Watu wawili wanahofiwa kupoteza maisha na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 16, 2013

TASWIRA :- Hali ilivyokuwa baada ya Bomu lililolipuka kwenye mkutano wa Chadema katika eneo la Soweto, huku Watu wawili wanahofiwa kupoteza maisha na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa.


Hali ilivyokuwa baada ya mlipuko.… huku Watu wawili wanahofiwa kupoteza maisha na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu lililolipuka kwenye mkutano wa Chadema katika eneo la Soweto, kata ya Kaloleni jijini Arusha, wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa madiwani katika maeneo ya jiji hilo  jana (juni 15,2013).



Hali ilivyokuwa baada ya mlipuko.… huku Watu wawili wanahofiwa kupoteza maisha na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu lililolipuka kwenye mkutano wa Chadema katika eneo la Soweto, kata ya Kaloleni jijini Arusha, wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa madiwani katika maeneo ya jiji hilo  jana (juni 15,2013).



Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akiwasili katika mkutano huo kwa helkopta.


Maelfu wakimpungia mikono Mbowe wakati akiwasili kwenye mkutano wa Chadema katika eneo la Soweto, kata ya Kaloleni jijini Arusha, wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa madiwani katika maeneo ya jiji hilo jana (Juni 15,2013).


Baada ya tukio hilo watu waliokuwa katika mkutano huo walitawanyika wakikimbia kuokoa maisha yao huku wakimwacha Mbowe na Lema na viongozi wengine wakiwa bado wako jukwaani.


Watu wawili wanahofiwa kupoteza maisha na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu lililolipuka kwenye mkutano wa Chadema katika eneo la Soweto, kata ya Kaloleni jijini Arusha, wakati wa Mkutano wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani mjini Arusha, jana (Juni 15,2013) .




Bomu hilo lililipuka jana saa 11:50 dakika chache kabla ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa,Bw. Freeman Mbowe kumaliza kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Soweto mjini Arusha na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi.




Hali ilivyokuwa baada ya mlipuko.
Hilo ni tukio la pili la bomu kulipuka katika mkusanyiko wa watu, kwani  Mei 5 mwaka huu bomu lililipuka katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasit mjini Arusha na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.




Habari kutoka eneo la tukio zimedai kwamba mlipuko huo ulitokea karibu na gari la matangazo la Chadema aina ya Mitsubishi Fusso lililokuwa jirani na jukwaa alilokuwa akilitumia Mwenyekiti wa Chama hicho,Bw. Freeman Mbowe jana jioni.



Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru Frida Mokiti amesema katika hospitali yake kuna maiti moja ya mtoto na majeruhi 11.




Habari zingine zilisema katika hospitali ya Misheni ya Selian kuna maiti za watu wawili, waliokufa kutokana na shambulio hilo na majeruhi ambao idadi yao haijafahamika.




Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas amesema katika tukio hilo watu wawili wamepoteza maisha, mwanamke na mwanamume na kwamba idadi ya majeruhi bado haijafahamika kwa kuwa wametawanywa katika hospitali mbalimbali mkoani humo.




Taarifa zilidai kuwa kuna mtu alionekana akirusha kitu kinachodaiwa bomu kwenye eneo la jukwaa karibu na gari la matangazo la chama hicho, lakini alipokuwa akifuatiliwa baada ya kutokea mlipuko huo, polisi nao walikuwa wameanza kudhibiti watu kwa kulipua mabomu ya kutoa machozi na kupiga risasi za moto hali iliyozidisha taharuki.




Baada ya tukio hilo watu waliokuwa katika mkutano huo walitawanyika wakikimbia kuokoa maisha yao huku wakimwacha Mbowe na Lema na viongozi wengine wakiwa bado wako jukwaani.




Hali hiyo ilifanya barabara zote za mji wa Arusha kujaa watu waliokuwa wakikimbia ovyo.




Hali hiyo ya watu kukimbia ovyo kuliwafanya askari polisi wengi kuingia mitaani kudhibiti watu na hivyo nao kulazimika kutumia mabomu ya machozi hali ambayo ilizidisha taharuki.




Baadhi ya watu waliojeruhiwa walikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru na wengine katika Hospitali ya Seliani na wafuasi wa Chadema na watu wengine waliokuwa katika eneo hilo.




Wafuasi wa Chadema.
Jana(Juni 15,2013)  Chadema ilikuwa ikifunga kampeni zake eneo hilo kusubiri uchaguzi mdogo wa udiwani ambazo zinafanyika sehemu mbalimbali nchini sambamba na uchaguzi mdogo wa ubunge Chambani, Pemba, Zanzibar.




Sambamba na Chadema pia vyama vya CUF na CCM vilifunga kampeni katika eneo hilo moja, wakati CUF iliyohutubiwa na Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba ikifanyika stendi ya mabasi ya Kampala Coach, huku CCM ikihutubiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye ilifunga kampeni zake katika kituo cha mabasi yaendayo Sanawari.




Mei 5,2013  takribani watu watatu walikufa katika Kanisa hilo nje kidogo ya Mji wa Arusha, na wengine kadhaa walijeruhiwa huku Balozi wa Vatican nchini na watawa waliokuwa katika shughuli maalumu ya kuzindua Parokia mpya ya Mtakatifu Yosefu walinusurika.




Aidha  Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi amesema mantiki ya demokrasia ya vyama vingi si kujenga chuki, uhasama na ugomvi bali ni shime ya ushindani wa nguvu ya hoja itokanayo na ushawishi wa kisera bila umwagaji damu na mfarakano.




Alhaji Mwinyi alitoa kauli hiyo jana, wakati akifunga kampeni za CCM katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mapape, Mkoa wa Kusini Pemba.




Kata 26 nchini leo(Juni 16,2013)  zinafanya uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi na madiwani kwa sababu mbalimbali. 



TAARIFA KUTOKA JESHI LA POLISI KUHUSU MLIPUKO WA BOMU JIJINI ARUSHA JANA,Juni 15,2013.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad